Pages


Home » » ZAIDI YA WAJASIRIAMALI 40 KUSHIRIKI MAONESHO YA UJASIRIAMALI - MBEYA

ZAIDI YA WAJASIRIAMALI 40 KUSHIRIKI MAONESHO YA UJASIRIAMALI - MBEYA

Kamanga na Matukio | 04:12 | 0 comments
Na mwandishi wetu
Zaidi ya wajasiliamali 40 kutoka Mbeya, Dar es salaam na Kenya watashiriki maonesho ya ujasiriamali yatakayofanyika kwa siku 3 katika viwanja vya shule ya msingi Ruanda Nzovwe jijini hapa.

Akiongea na mwandishi wetu meneja masoko wa Mbeya Trade Fair bwana Stephen Msekwa amesema nia ya kuchanganya wajasilia mali wa ndani na nje ya nchi ni kuwaongezea ujuzi wajasilia mali wa ndani katika shughuli zao.

Amezitaja bidhaa zitakazo oneshwa siku hiyo kuwa ni nguo za asili, wine, sabuni za kuongea, sabuni za usafi wa choo na juisi.

Aidha amesema maonesho hayo yanatarajiwa kufunguliwa November 4 na mkurugenzi wa jiji la Mbeya Juma Idi na kufungwa November 6 na mkuu wa mkoa wa Mbeya Abasi Kandoro.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger