Pages


Home » » Wachimbaji wa Madini watakiwa kutumia Teknolojia za kisasa ili kuepukana na hasara wanazozipata katika uzalishaji.

Wachimbaji wa Madini watakiwa kutumia Teknolojia za kisasa ili kuepukana na hasara wanazozipata katika uzalishaji.

Chimbuko Letu | 10:18 | 0 comments
Na Ezekiel Kamanga,Chunya.

Chama cha wachimba madini mkoani Mbeya tawi la Chunya(Mberema)wametakiwa kuachana na kuchimba madini kwa mazoea badala yake watumie Teknolojia za kisasa ili kuepukana na hasara wanazozipata katika uzalishaji.

Haya yameelezwa na mawakala wa  Jiolojia Tanzania(GST) kutoka Dodoma  katika kikao cha chama cha wahimba madini tawi la Chunya (mberema) Kilichokuwa kikiongozwa na mwenyekiti wa wachimba madini mkoa wa Mbeya Leonard Manyesha,wakati wataalamu hao wakitoa elimu juu utafiti wa miamba  kwa kutumia vifaa vya kisasa ili kubaini uwepo wa madini  wanayoyatafuta.

Wakitoa mada kwa wachimbaji madini kwa njia ya kisansi mjiolojia  Alphoncce Michael na mjiofizikia Octavian Minja walisema utafutaji wa madini kwa njia ya jiolojia hutumika kuanisha miamba na madini kwenye eneo husika na  kupata taarifa kwa haraka zaidi na hupunguza gharama za uendeshaji kwa kuokoa muda na kujua uwepo wa madini au laa.

Walisema baada ya kufanya tafiti mchimbaji anaweza kujua ni nini afanye ili aweze kupata kile anachokihitaji kwani wamedai kuwa njia za asili za kutazama kwa macho kwa kuangalia aina ya udongo zinachua muda mrefu na hutumia nguvu nyingi na gharama huwa kubwa bila kujua kama anchokitafuta atakipa ipasavyo.

Aidha wachimbaji waliohudhulia kikao hicho walisema waliwashukuru mawakala hao wa jiolijia kwa kuwaletea  elimu hiyo ya uchimbaji wa kisasa na kuomba ofisi ya madini kwa kushirikiana na  halmashauri ya wilaya ya chunya ieweze kuwasaidia  kuhakikisha  mitambo hiyo ya  kufanyiwa utafiti inawafikia wachimbaji kwenye maeneo yao ya kazi ili kuhakikisha wanafanya kazi kwa manufaa.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger