Pages


Home » » WATENDAJI WA HALMASHAURI NA WILAYA WAMETAKIWA KUONDOA URASIMU WA TAARIFA KWA WAANDISHI WA HABARI MBEYA.

WATENDAJI WA HALMASHAURI NA WILAYA WAMETAKIWA KUONDOA URASIMU WA TAARIFA KWA WAANDISHI WA HABARI MBEYA.

Kamanga na Matukio | 03:29 | 0 comments
Waandishi wa habari wakongwe na waliobobea mkoani Mbeya
*****
Na mwandishi wetu
Katibu tawala msaidizi Utumishi na Utawala Bwana Leonald Magacha amewataka watendaji wa halmashauri na wilaya kuondoa urasimu wa taarifa kwa waandishi wa habari ili kuiwezesha jamii kutambua mambo yanayoendelea katika mkoa wao.

Ameyasema hayo kufuatia kuwepo kwa tabia ya baadhi ya wakuu wa idara kutoka halmashauri mbalimbali kutokuwa na ushirikiano na vyombo vya habari katika kutoa taarifa hali inayowalazimu waandishi wa habari kutafuta njia mbadala ya kupata habari hizo.

Naye mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Mbeya Christopher Nyenyembe ameuomba uongozi wa Serikali mkoani hapa kuondoa ubaguzi wa vyombo vya habari katika kutoa taarifa ili kuondoa hisia binafsi za mtu katika utendaji kazi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger