Pages


Home » » WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI BESTA (ENGLISH MEDIUM) WAONDOLEWA SHULENI BAADA YA SHULE KUUZWA KWA AMRI YA MAHAKAMA MBEYA

WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI BESTA (ENGLISH MEDIUM) WAONDOLEWA SHULENI BAADA YA SHULE KUUZWA KWA AMRI YA MAHAKAMA MBEYA

Kamanga na Matukio | 03:12 | 0 comments

 Hii ndiyo Shule ya Msingi ya Besta Sae Mbeya.
  
 Vibarua waliopewa jukumu la kuhamisha mizigo shuleni hapo
 Viti  vikiwa vimetolewa eneo la shule ya Msingi Besta
 Gari la mizigo likichukua mizigo kuelekea eneo Jengine
 Waliopewa Dhamana ya kuchukua mizigo wakiwa  wanaingia ndani kwa nguvu kutoa vitu katika shule hiyo ya Besta
 Wanafunzi wa Shule ya Besta wakiwa Hawaelewi cha kufanya wakati mizigo yao aikichukuliwa

 Mmiliki wa Kampuni ya Ulinzi  ya Retired Army Bwana Kubaja akiimarisha ulinzi baada ya kupewa jukumu la kulinda shule hiyo na Wamiriki wapya.
 Kipande cha Shule ya Besta
 Polisi wakiwa na watu waliopewa dhamana ya kutoa vitu Besta wakiwa wanaendelea kutoa vitu hivyo
 Baadhi ya vitu ambavyo vilitolewa nje ya Shule ya Besta
Vijana waliopewa Dhamana ya kutoa vitu vya Shuleni hapo wakitoa Magari nje ya Shule hiyo
 Msikiti ambao upo ndani ya shule ya Msingi Besta ambao pia wananchi wa Jirani wanatumia , nao pia umenunuliwa kwa Amri ya Mahakama
 Wanafunzi wa Shule ya Msngi ya Besta wakiwa Bado hawajui cha kufannya

 Wanafunzi wa Shule ya Msingi wa Besta wakiwa wanakusanya Madftari yake pamoja na Mitihani yao.

 Mmiriki wa Shule ya Besta Ndugu Hamis Othnman akimsihi Askari ampe nakala ya kuondolewa kwake Shuleni Hapo.
  Mmiriki wa Shule ya Besta Ndugu Hamis Othnman akikataliwa na Askari hoja yake yakupewa nakala ya kuondolewa kwake na kutakiwa kumuona Mkuu wa kituo cha Polisi kati au Kumuona msajili wa Mahakama Kuu


***************
Na Ezekiel Kamanga
Mahakama kupitia dalali wa Mahakama imepiga mnada Shule ya Msingi Besta iliyopo Sae jijini Mbeya kutokana na madai ya mdai katika kesi hiyo .
Mdai wa kesi hiyo namba 212 ya mwaka 2003 ni Kampuni ya Mohamed Enterprises ambapo alikuwa anamdai Hamis Othman kiasi cha Shilingi Milioni 270 ambazo alishindwa kulipa . 
Kesi hiyo namba 27 ilianza kusikilizwa mwaka 2003 huku Othman  akitetewaa na Wakili Mkumbe ambapo hukumu ilitolewa 4.6.2012  majengo ya shule yauzwe, mpaka sasa madai hayo  hayaja jurikana yalikuwa yanahusiana na nini.
Wamiliki wapya wa majengo  hayo ni Mbeya Heritage Company ambao walikabidhiwa majengo hayo na Dalali wa Mahakama Chini ya usimamizi wa mtendji kata ya Ilomba Erasto Mwakapoma  na Mwenyekiti waa Mtaa wa Sae Erias Mwakyusa huku  Jeshi la Polisi Likishuhudia makabidhiano hayoyakifanyika kwa amani.
Zoezi lilisitishwa kwenye Msikiti kutokana na Imani waumini wa Msikiti huo wataalifiwe ili ndani ya siku Mbili wawe wameondoka eneo hilo. 
Adha kubwa ilikuwa ni kwa wanafunzi wliokuwepo shuleni hapo ambapo mitihani yao ilioekana kuzagaa hovyo kutokana  na purukushani zilizo kuwepo bila taarifa yoyote na kutojua Hatma yao  ya masomo yao kutokana na Madarasa kuhodhiwa  na mmiliki mwengine Licha ya kuwepo kwa mabweni kando ya Shule hiyo na kufanya mizigo yote kulundikwa nje ya mabweni.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger