Pages


Home » » SAKATA LA HUNDI ZA MIRATHI KUTOWAFIKIA WAHUSIKA.

SAKATA LA HUNDI ZA MIRATHI KUTOWAFIKIA WAHUSIKA.

Kamanga na Matukio | 04:15 | 0 comments
Na mwandishi wetu
Imedaiwa kuwa hundi nyingi za mirathi zimekuwa haziwafikii warithi na kubaki mahakamani kutokana na mawasiliano duni kati ya msimamizi wa mirathi na mahakama za mwanzo

Aidha warithi kutochukuwa hundi kutokana na kukata tama inayosababishwa na kutokuwa na taarifa ya kukamilika kwa malipo, gharama za kufuata malipo kuwa kubwa na urasimu wa watendaji wa mahakama.

Hayo yamebainishwa na afisa mirathi kutoa hazina bwana Wiliamu Kesi wakati akitoa mafunzo ya kukabilia na changamoto hizo kwa watendaji na mahakimu wa mahakama za mwanzo kwa mikoa ya Iringa na Ruvuma.

Wakati huohuo amezitaka familia kumteua msimamizi anayeaminika na familia kwa ujumla ili kuondoa tofauti zinazoweza kujitokeza wakati wa kufuatilia mirathi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger