Pages


Mganga maarufu wa jadi aliyefamika kwa jina la Shija Ndula Jinan’gai kuamua kusalimisha matunguli yake katika Kanisa la Nyumba ya Maombi(House of Prayer Shield of faith) Pambogo Kata ya Iyela jijini Mbeya.

Chimbuko Letu | 08:21 | 0 comments


Mganga maarufu wa jadi aliyefamika kwa jina la Shija Ndula Jinan’gai(35)mkazi wa Mapogolo Kata ya Madibira Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya ameachana na kazi hiyo na kuamua kusalimisha matunguli yake katika Kanisa la Nyumba ya Maombi(House of Prayer Shield of faith) Pambogo Kata ya Iyela jijini Mbeya.


Shija Ndula mwenye familia ya Mke na watoto wanne ambaye sasa anafahamika kwa jina la Mussa Shija amesema ameitumikia kazi hiyo takribani miaka saba kabla ya kuamua kuachana na kazi hiyo  na kujiunga na Kanisa linaloongozwa na Mchungaji Isaya Laiser chini ya Kiongozi wake Mkuu Nabii Mulilege Mkombo maarufu(Mzee wa Yesu) kutokana na kutopata mafanikio katika uganga wa kienyeji.

Akiongea kwa ujasiri mganga huyo amesema kuwa kazi aliyokuwa akiifanya kwa muda wote huo hakupata mafanikio yoyote licha ya kutoza fedha nyingi kwa wateja wake kuanzia shilingi laki moja hadi milioni mbili ambazo alizitumia kwa anasa tu.

Hata hivyo mke wa mganga huyo Debora Mwandu(30) amesema kuwa yeye anamshukuru Mungu kwa maisha mapya ndani ya Yesu kwani mganga ambaye ni mume wake aliacha kazi yake ya ufundi wa kushona nguo akidai hapati faida yoyote na kujiingiza kwenye uganga akidai kuwa mizimu imemwambia huko ndiko kwenye mafanikio.

Pamoja na kufanya kazi hiyo kwa miaka saba hakuwahi kununua uwanja wa kujenga nyumba wala kuweka akiba benki huku mambo yao yakienda mrama kutokana na mapato najisi ambapo wateja wake wengi walikuwa ni wahalifu wakiwemo majambazi ambao walikuwa wakiomba dawa ili wafanikiwe katika uhalifu.

Baadhi ya wateja walikuwa wanandoa,wanasiasa na wafanyabiashara ambao walikuwa wakihitaji dawa kwa ajili kuboresha biashara zao lakini alijua kuwa huo ulikuwa ni utapeli ambao ulikuwa unamkosanisha na Mungu.

Hata hivyo katika kazi hiyo mganga huyo alikutana na changamoto kutoka kwa walimu wake ambao walidai kuwa ili kuongeza umaarufu ni vema kutumia viungo vya bindamu hali iliyomkosesha amani kutokana na mauaji ya banadamu jambo ambalo amepingana nalo na kuamua kumwishia Yesu.

Vitendo hivyo pia viliendana na matumizi ya wanyama pori ambazo ni nyara za Serikali  kama mafuta ya Simba au ngozi za wanyama hali ambayo aliona ni hatari kwa maisha yake kwani wakati wowote angeweza kukumbana na mkono wa sheria.

Mganga huyo ametoa wito kwa waganga wa kienyeji kuachana na kazi hiyo kwani haina tija kwa jamii pia huleta uchonganishi kwa jamii na kusababisha mauaji  yasiyo ya lazima kwa jamii isiyo na hatia wakiwamo walemavu wa ngozi.

Aidha ametoa rai kwa wananchi kwamba hivi sasa waganga hao wamenda mbali zaidi kwa kudai kujihusisha na mtandao wa free mason kwa kudai kuwaondolea umaskini watu huku wakiwatoza fedha nyingi na wananchi wengi hutapeliwa kwa matumaini ya kupata utajiri.

Kwa upande wake Mchungaji Laiser wa Kanisa la nyumba ya maombi amesema ujio wa mganga huyo ni kufuatia mfungo wa mwezi mzima ukiokuwepo kanisani kwake hivi karibuni,aidha amesema Kanisa lina mpango wa kumnunulia cherehani ili aendelee kushona  aweze kujikimu kimaisha.

Mussa Shija alimaliza kwa kutoa wito kwa waganga wa kienyeji kuachana na mila potofu za uchonganishi kwa jamii ili kuleta amani katika jamii,Mkoa na Taifa kwa ujumla.





















WANAWAKE WAMETAKIWA KUJITOKEZA KUPIMA AFYA ZAO ILI KUEPUKANA NA UGONJWA WA SHINGO YA KIZAZI

Chimbuko Letu | 07:49 | 0 comments
 Picha hii imetumika kupamba habari, lakini haijachukuliwa katika eneo husika la habari hii.
 
 
Na Ezekiel Kamanga.
Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ileje Mkoani Mbeya Daktari Gerald Yubaha amewataka wanawake kujitokeza kwa wigi katika zahanati,vituo vya Afya na Hospitali ili kupima afya zao ili kubaini na kuondoa ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi Wilayani humo.

Yubaha ameyasema hayo katika maadhimisho ya siku ya wauguzi Duniani iliyofanyika Kiwilaya katika Hospitali ya Wilaya iliyopo Itumba Mei 12 mwaka huu ambapo Wauguzi na wahudumu wa Afya walifanya maandamano ya kumkumbuka Muuguzi wa kwanza Duniani ambapo maandamano hayo yalipokelewa na Mkuu wa Wilaya Rosemary Senyamule.

Kaimu Mganga Mkuu amesema kuwa baadhi ya changamoto ni pamoja na ukosefu wa mashine za kupimia vipimo katika Wilaya ambazo zingebaini magonjwa mbalimbali yakiwemo ya shingo ya uzazi kwa akina mama kwani kwa sasa huduma hiyo huipata katika hospitali ya wazazi Meta iliyopo Jijini Mbeya na Hospitali yake hutumia gharama kubwa kuwasafirisha wagonjwa wanaowabaini.

Tangu kuanza kutolewa elimu ya ugonjwa wa shingo ya uzazi wagonjwa wanne walibainika na ugojwa huo ambapo wawili kati yao walifariki kutokana na kuchelewa kupata matibabu na wawili walisafirishwa hadi Mbeya ambapo wanapatiwa matibabu katika Hospitali ya Wazazi ya Meta.

Katika maandamano wauguzi hao walibeba mabango mbalmbali ili kufikisha ujumbe kwa serikali ambayo baadhi yakidai malimbikizo ya stahiki mbalimbali wanazodai watumishi wa sekta ya Afya ambayo hayajalipwa kwa muda mrefu.

Akijibu kero hizo za Wauguzi Mkuu wa Wilaya alisema Serkali imejitahidi siku hadi siku kuhakiksha wanalipa malimbikizo yao kwa wakati kadri fedha zinapopatikana kwani serikali haipo tayari haipo tayari kuona watumishi wake wanaishi maisha duni.

Alisema Serikali ina majukumu mengi ikiwa ni pamoja na upanuzi wa Hospitali hiyo ambapo ujenzi unaendelea ili kuwaondolea adha ya wananchi wa wilaya hiyo badala ya kusfiri umbali mrefu na wengi hupoteza maisha kwa kukosa gharama za kuwasafirisha ndugu zao wanapokuwa wanahitaji matibabu zaidi Mbeya.

Aliwataka kuendelea kuwa wavumilvu na kuwapongeza kwa moyo wa uzalendo ambao wamekuwa wakifanya wa kutoa huduma licha ya kufanya kazi katika mazingira magumu na kuwajali wagonjwa wanaofika hosptalini kwa ajili ya kupata huduma.
 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger