Pages


Home » » WANANCHI WATAKIWA KUVITUNZA VYAZO VYA MAJI NYIMBILI WILAYANI MBOZI MBEYA

WANANCHI WATAKIWA KUVITUNZA VYAZO VYA MAJI NYIMBILI WILAYANI MBOZI MBEYA

Kamanga na Matukio | 03:30 | 0 comments
Na mwandishi wetu.
Wananchi waishio kandokando ya vyanzo vya maji wametakiwa kuvitunza vyanzo hivyo ili kusaidia kupatikana kwa maji katika kipindi chote cha mwaka

Rai hiyo imetolewa na wakulima wanaojishughulisha na kilimo cha umwagiliaji katika bonde la Chizumbi lililopo kata ya Nyimbili wilayani Mbozi mkoani Mbeya.

Wamesema endapo vyanzo hivyo vitatunzwa kikamilifu vitasaidia kuondokana na tatizo la maji pamoja na kuiwezesha mito kutiririsha maji kwa kipindi chote cha mwaka

Mmoja wa wakulima hao Bi.Sophia Kayombo ametoa ombi kwa serikali kuwatafutia soko la mazao yao ili waweze kunufaika zaidi na kilimo hicho

Bonde la Chizumbi limekuwa chachu ya maendeleo kwa wakulima katika kilimo cha umwagiliaji kwa zao la mpunga, mahindi na mbogamboga kwa wilaya ya Mbozi na Ileje.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger