Pages


Home » » (CCM) Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya kimeanza kuwajengea uwezo viongozi wake.

(CCM) Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya kimeanza kuwajengea uwezo viongozi wake.

Chimbuko Letu | 10:20 | 0 comments
Na Ezekiel Kamanga, Kyela.
 
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya kimeanza kuwajengea uwezo viongozi wake kuanzia ngazi ya kitongoji, kijiji, matawi na Kata ili kusaidia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi mkuu uliopita.
 
Akizungumza na Kituo hiki, Katibu wa Siasa, Itikadi na Uenezi wa CCM Wilaya ya Kyela, Richard Kilumbo alisema zoezi hilo lilianza mwezi machi na linatarajiwa kukamilika Aprili mwaka huu.
 
Alisema lengo la mafunzo kwa viongozi wa matawi, vitongoji, vijiji na Kata wa Chama cha mapinduzi ni kuwajengea uwezo juu ya namna ya kusaidiana na uongozi wa serikali katika kutatua kero mbali mbali katika jamii pamoja na kusaidia utekelezaji wa ahadi zilizotolewa kwenye uchaguzi mkuu 2015.
 
Alisema Wilaya hiyo yenye vitongoji zaidi ya 300, vijiji 101 na Kata 37 itasaidia viongozi hao kuwa kiungo kizuri kati ya Chama na Serikali ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa jamii.
 
“Lengo letu tunataka kuwe na mahusiano mazuri baina ya wananchi, Serikali iliyopo madarakani na Chama kuanzia ngazi ya chini ya tawi kwani hili litasaidia sana kusukuma gurudumu la maendeleo ili kwendana na kasi ya Rais” alisema Katibu huyo.
 
Aliongeza kuwa endapo viongozi hao watakuwa na maelewano mazuri na uongozi wa Halmashauri kwa kushirikiana na Madiwani waliopo itasaidia kuisimamia serikali katika utekelezaji wa miradi mbali mbali katika maeneo yao.
 
Alisema mara nyingi viongozi wa serikali hawana mahusiano mazuri na uongozi wa chama katika ngazi za chini jambo linalosababisha kutokuwa na maendeleo pamoja na miradi mbali mbali kukwama.
 
Katibu huyo alisema lengo linguine la mafunzo hayo ambayo wahusika hufuatwa kwenye maeneo yao ni kuondoa makando kando ya uchaguzi uliopita kwa kile alichodai bado kuna mgawanyiko baina ya wanachama na viongozi.
 
“pia ikumbukwe kuwa katika kipindi cha uchaguzi kulikuwa na matabaka ambayo sio kweli kuwa yameisha licha ya kuhubiriwa kwenye majukwaa lakini tunachofanya sasa ni kuelezana madhara ya mgawanyiko katika shughuli za maendeleo kwa jamii tunayoiongoza” alisema Katibu.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger