Pages


Home » » MKUU WA MKOA WA MBEYA MH KANDORO AWATAKA WANANCHI KUTOKUWA NA JAZBA, CHUKI KATIKA UCHANGIAJI WA MAONI YA KATIBA MPYA WAKATI UTAKAPOFIKA.

MKUU WA MKOA WA MBEYA MH KANDORO AWATAKA WANANCHI KUTOKUWA NA JAZBA, CHUKI KATIKA UCHANGIAJI WA MAONI YA KATIBA MPYA WAKATI UTAKAPOFIKA.

Kamanga na Matukio | 05:24 | 0 comments
Mkuu wa mkoa wa Mbeya mheshimiwa Abbas Kandoro
*****
Na mwandishi wetu
Mkuu  wa Mkoa wa Mbeya Bw Abbas Kandoro amesema kuwa wakati utakapokuwa umefika  wa kukusanya maoni  ya katiba mpya wananchi wanatakiwa kutotumia jazba, chuki au shinikizo kwani katiba hiyo ni sheria mama inatakiwa kujadiliwa kwa umakini.

 Mkuu huyo wa Mkoa alisema hivi sasa suala la katiba  mpya linazungumzia karibu kila kona hivyo kuna umuhimu likapewa umuhimu wa aina yake na likajadiliwa kwa kina na si kujadili wakati wananchi wakiwa na chuki zao au shinikizo.

Alisema kuwa matatizo yaliyopo hivi sasa mkoani hapo ni ya mpito,kwa kuwa hakuna taifa linalojengwa kwa mara moja isipokuwa ni kwa kuunganisha nguvu kama taifa ili kuona ni namna gani matatizo hayo yatakabiliwa.

Bw. Kandoro alisema kuwa suluhisho la matatizo hayo haliwezi kutatuliwa kwa kufanya fujo wala kupiga watu nondo bali huo ni uhalifu ambao haustahili kushabikiwa kamwe.

  Aidha Bw.Kandoro alitumia nafasi hiyo kuwaasa wananchi wa Mbeya kushiriki kikamilifu katika mchakato wa Katiba mpya utakapoa anza kwa kutoa mawazo yao ili kuboresha katiba hiyo kwa manufaa ya Taifa ni ya Mtu moja mmoja.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger