Pages


Home » » DIWANI NA AFISA MTENDAJI WA KATA YA RUIWA MKOANI MBEYA WAKACHA MKUTANO.

DIWANI NA AFISA MTENDAJI WA KATA YA RUIWA MKOANI MBEYA WAKACHA MKUTANO.

Kamanga na Matukio | 05:49 | 0 comments
 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) mheshimiwa Hamad Sharifu awataka Diwani na Afisa mtendaji wa kata ya Ruiwa kuwasikiliza wananchi kero zinazowakabili katika shughuli za maendeleo katika kata hiyo iliyopo wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya.
Baadhi ya wananchi wa kata ya Ruiwa. wilayani Mbarali wakitaka kusomewa taarifa za mapato na matumizi ambapo diwani wa kata hiyo ni Bwana Alex Ndamlage na Afisa mtendaji ni Bwana Jordan Masweve ambayo kwa pamoja wanadaiwa kukwepa kukutana na wananchi amabo wanadai kusomewa taarifa za mapato na matumizi licha kukusanya pesa kibao za mifugo.

Kwa pamoja viongozi hao wa kata walimkamata na kumweka mahabusu mmoja wa wananchi hao Bwana Juma Merere kuanzia majira ya saa 10 usiku wa manane hadi saa 4 asubuhi ambaye alikuwa akisambaza taarifa na mkutano huo wa kutaka kusomewa mapato na matumizi, hali iliyopelekea wananchi kutishia kuvunja ofisi ya mifugo ambayo walimfungia mwananchi huyo ndipo walipomuachia Bwana Juma nawao kutokomea.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger