Pages


Home » » MELI YA MV SONGEA YASIMAMISHA SAFARI ZAKE BAADA KUHARIBIKA ILI IFANYIWE MATENGENEZO.

MELI YA MV SONGEA YASIMAMISHA SAFARI ZAKE BAADA KUHARIBIKA ILI IFANYIWE MATENGENEZO.

Kamanga na Matukio | 01:11 | 0 comments
Na mwandishi wetu.
Meli ya MV Songea inayosafirisha abiria na mizigo katika maeneo mbalimbali ndani ya ziwa Nyasa, imesimamisha safari zake baada ya kuharibika ili ifanyiwe matengenezo.

Kwa sasa meli hiyo imeegeshwa katika bandari mpya ya Kiwira wilayani Kyela ikisubiri kwenda kufanyiwa matengenezo katika bandari ya Drydock nchini Malawi.

Meneja wa kampuni ya Marine Services inayomiliki meli hiyo, Baraka Bigambo amesema meli hiyo imetoboka sakafu na imeanza kuingiza maji halki inayohatarisha usalama wa abiria na mali zao.

MV Songea inao uwezo wa kubeba abiria 200 na tani 50 za mizigo na inatoa huduma katika ukanda mzima wa pwani ya upande wa Tanzania na nchi jirani ya Malawi.

Meli ya Mv Iringa ndiyo inayoendelea kutoa huduma za usafirishaji ambapo meli hiyo inauwezo wa kubeba abiria 138 na tani 15 za mizigo.

Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya Bandari wilayani Kyela, Absalum Bohela amesema kuharibika kwa meli hiyo kumeathiri Mamlaka ya Bandari kutokana na kukosa mapato yatokanayo na shughuli zinazofanywa na meli hiyo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger