Pages


Home » » MTOTO AJERUHIWA BAADA YA KUPINGWA NA WATU WANAODAIWA KUWA NI MAJAMBAZI

MTOTO AJERUHIWA BAADA YA KUPINGWA NA WATU WANAODAIWA KUWA NI MAJAMBAZI

Kamanga na Matukio | 06:26 | 0 comments
 Mtoto Victa Tobia aliyejeruhiwa baada ya kupingwa na watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi
Na mwandishi wetu
Mtoto Victa Tobias mwenye umri wa miaka 12 mkazi wa Kamficheni Soweto jijini Mbeya amepigwa na watu wasiofahamika asubuhi ya jana baada ya kudhaniwa kutaka kuiba vyuma chakavu kwenye moja ya gereji jijini hapa.

Kutokana na kipigo hicho mtoto huyo amejeruhiwa katika sehemu mbalimbali za mwili wake na kusababisha uvimbe katika maeneo ya mabega, mgongoni na kichwani.

Mwenye wa mtaa Ruanda Sinde bwana Patrik Haule amesema mtoto huyo amepigwa kwa kuhisiwa kuwa ni mwizi wa vyuma chakavu na kwamba amechukuliwa na kupelekwa katika hospitali ya Rufaa Mbeya kwa ajili ya matibabu kutokana na hali yake kuwa mbaya.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger