Pages


Home » » MATOKEO YA UCHAGUZI WA CCM MKOANI MBEYA... PROFESA MWANDOSYA AIBUKA KIDEDEA NAFASI YA MNEC RUNGWE. .

MATOKEO YA UCHAGUZI WA CCM MKOANI MBEYA... PROFESA MWANDOSYA AIBUKA KIDEDEA NAFASI YA MNEC RUNGWE. .

Kamanga na Matukio | 02:47 | 0 comments
Na Solomon Mwansele, Mbeya..
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais (Kazi Maalum), Profesa Mark Mwandosya, ameibuka kidedea katika kinyang'anyiro cha kuwania nafasi ya Ujumbe Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa (CCM), wilaya ya Rungwe.

Profesa Mwandosya alifanikiwa kuwaacha kwa mbali wapinzani wake wawili waliojitokeza kuwania nafasi hiyo.

Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi huo, Mkuu wa wilaya ya Kyela, Magareth Mahenga, akitangaza matokeo hayo, alisema Profesa Mwandosya ameibuka mshindi katika nafasi ya NEC kwa kupata kura 1,118.

Kada maarufu aliyejitokeza kuwania nafasi hiyo, Richard Kasesela, alijikuta akiambulia kura 198 huku, Asobenye Mwandiga, ambaye naye aliingia katika kinyanyiro hicho cha nafasi ya NEC akijikuta akiambulia kura 28.

Kwa mujibu wa Magareth jumla ya kura za wajumbe walioshiriki uchaguzi huo mkuu wilaya ya Rungwe walikuwa 1,344 ambapo kura halali zilikuwa 1,354 wakati kura 12 ziliharibika.

Magareth alisema nafasi ya Mwenyekiti wa CCM wilayani humo, imenyakuliwa na Ally Mwakalindile kwa kupata kura 948, akiwatupa pembeni wapinzani wake Samwel Mwakyambiki aliyepata kura 469 huku Antony Mwanjejele akipata kura 44.

Nafasi za wajumbe kumi wa halmashauri Kuu ya CCM wilaya zilichukuliwa na Esther Mwakipesile, Richard Kasesela, Burton Mwakasendo, Isabela Mwambela, Hawa Abdul, Amon Angetile, Twalim Mwaijumba, Michael Pascal, John Mwakifuna na Rapael Ngeko.

Aliwataja wajumbe wawili wa mkutano mkuu wa CCM mkoa waliochaguliwa kutoka wilaya ya Rungwe kuwa ni Dorith Kimambo na Michael Pascal.

Katika nafasi za wajumbe watano wa mkutano mkuu wa CCM Taifa, waliochaguliwa ni Salome Mwakalinga, Richard Kasesela, Lutengano Mwalwiba, Petro Pareso na Meckson Mwakipunga.

Wakati huo huo  Bwana Mathayo Mwangomo, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilaya ya Mbarali baada ya kuwashinda wapinzani wake wawili waliokuwa wamejitokeza kuwania nafasi hiyo.

Mwangomo alifanikiwa kuibuka kidedea katika nafasi hiyo kwa kupata kura 541, na kuwashinda Ignas Mgao aliyepata kura 429 huku Benedict Masuvha akiambulia kura 76.

Msimamizi Mkuu wa uchaguzi huo, Florence Kyendesya, alisema jumla ya kura zilizopigwa zilikuwa ni 1,080 wakati kura halali zilikuwa 1,046 ambapo jumla ya kura zilizoharibika zilikuwa ni 34.

Nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), ilichukuliwa na Geofrey Mwangulumbi kwa kupata kura 596 akiwashinda wapinzani wake Paul Kitha aliyepata kura 261 huku Hanji Godigodi akiambulia kura 137.

Florence aliwataja wajumbe wawili wa mkutano mkuu wa CCM mkoa waliochaguliwa kuwa ni Bruno Mgumba na Martin Mdenye.

Mkuu wa wilaya ya Mbarali, GullamHussein Kifu, aliongoza kwa kupata kura nyingi katika nafasi za wajumbe weatano wa mkutano mkuu wa CCM Taifa, na wengine waliochaguliwa ni Yusuph Mwaipalu, Muhenza Mlwilo, Salome Stemile na Feinti Mwashikumbulu.

Kwa upande wa nafasi kumi za wajumbe wa halmashauri Kuu ya CCM wilaya walioibuka kidedea ni Zamoyoni Mhanji, Hanji Godigodi, Amadi Njolombe, Defesi Kihombo na  Ambindwile Mwaijumba.

Wajumbe wengine waliochaguliwa katika nafasi hiyo ni Eliud Mahenge, Feinti Mwashikumbulu, Cliford Mwakiholano, Abdul Mulla na Jeremiah Kadenge.

 MBEYA MJINI

EPHRAIM Mwaitenda amechaguliwa kwa kishindo, kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilaya ya Mbeya mjini baada ya kuwabwaga vibaya wapinzani wake wawili waliokuwa wanawania nafasi hiyo.

Mwaitenda aliibuka kidedea kwa kupata kura 552, huku Emili Mwaluka akishika nafasi ya pili kwa kura 142 wakati nafasi ya tatu ilichukuliwa na Japhet Mwasanga aliyeambulia kura 108.

Katibu wa CCM wilaya ya Mbeya mjini, Raymond Mwangwala, akizungumza na gazeti hili alisema uchaguzi huo uliofanyika uwanja wa Sokoine mjini hapa, ulihudhuriwa na wajumbe 1,016 na ulikuwa na utulivu mkubwa.

Mwangwala alisema katika nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), wilayani ilichukuliwa na kada maarufu Sambwee Shitambala, aliyepata kura 653 na hivyo kufanikiwa kuwabwaga kwa mbali Kamanda wa UVCCM mkoa, Dk.Stephen Mwakajumilo aliyepata kura 278, Fatuma Kasenga aliyepata kura 67 na Daniel Fussi aliyeambulia kura 17.

Kwa nafasi ya wajumbe wawili wa mkutano mkuu wa CCM mkoa, waliochaguliwa ni mwandishi wa habari wa kituo cha redio cha Generation Fm, kilichopo mjini Mbeya, Jackson Numbi na Tonebu Chaula.

Katibu huyo wa CCM wilaya ya Mbeya mjini, aliongeza mwandishi wa habari wa kampuni ya Business Times, mkoa wa Mbeya Charles Mwakipesile, aliibuka kidedea kwa kupata kura 630 katika nafasi ya wajumbe kumi wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya.

Wengine walioshinda katika nafasi hiyo ni Fatuma Kasenga, Edina Mwaigomole, Odran Chaula, Benjamin Balali, Henje Mwalungwe, Maria Nyagawa, Isaack Sintufye, Godfrey Habaya na mmliki wa kituo cha redio cha Generation Fm, Shadrack Makombe.

Mwangwala alisema wajumbe watano wa mkutano mkuu wa CCM Taifa walioibuka kidedea ni Charles Mwakipesile, Hamis Koko, Shadya Mtoro, Christina Gwimile na Frank Mahemba.

WILAYA YA CHUNYA.

CHAKUPEWA Makelele amefanikiwa kutetea nafasi yake ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilaya ya Chunya baada ya kumshinda mpinzani wake mkubwa Noel Chiwanga.

Makelele alishinda nafasi hiyo kwa kupata kura 785, huku mpinzani wake Chiwanga akimsogelea kwa karibu kwa kuambulia kura 716.

Akitangaza matokeo hayo, msimamizi mkuu wa uchaguzi huo, ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Ileje, Rosemary Sanyamule, alisema uchaguzi huo ulikwenda vizuri licha ya kuchelewa kuanza kutokana na ajali iliyosababisha kifo cha kada wa CCM, Issaya Nchimbi (45), aliyefariki dunia baada ya gari alilokuwemo kupindukia mtaroni.

Rosemary alisema Naibu Waziri wa Elimu ya Ufundi na Mafunzo, Philipo Mulugo, aliibuka kidedea katika nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC),kwa kupata kura 1034 huku wapinzani wake Polcap Ntapanya akipata kura 314, wakati Hamadi Juma aliambulia kura 96.

Katika nafasi ya wajumbe wawili wa mkutano mkuu wa CCM mkoa, waliochaguliwa ni Edina Mwangoka na Frank Chonya.

Rosemary alisema wajumbe kumi wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya waliochaguliwa ni Damson Nthangu, Antigon Kavishe, Edina Mwangoka, Anyangile Mwaipungu, James Mwanitenga, Bruno Mbegeze, Zaituni Sembo, Remji Sasun, Phide Mwalukasa na Wankunda Bangubangu.

Wajumbe watano wa mkutano mkuu wa CCM Taifa walioibuka kidedea wilayani Chunya ni Mkuu wa wilaya ya Chunya, Deodatus Kinawiro, Sauli Mwaisenye,  Polcap Ntapanya, Frank Chonya na Sophia Mwanauta.

WILAYA YA MOMBA:-
JUMA Rashid ameibuka kidedea katika nafasi ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilaya mpya ya Momba baada ya kuwashinda wapinzani wake wawili waliojitokeza kugombea nafasi hiyo.

Rashid alipata kura 333 akifuatiwa na Antony Mayega aliyepata kura 254 huku Nebath Simbeye akiambulia kura 245.

Msimamizi wa uchaguzi huo, Mwanaidy Mgogo, alisema uchaguzi huo ulikwenda vizuri licha ya kuwa nusura uingie dosari baada ya wajumbe kuanza kugonga madirisha baada ya kuchelewa kutangazwa kwa matokeo.

Mwanaidy alisema mjumbe wa NEC aliyechaguliwa ni Jackson Mbwile kwa kupata kura 338, akiwaacha Leonard Simbeye aliyejizolea kura 236 huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na Fotunartus Simfukwe aliyepata kura 189.

Aliongeza wajumbe watano waliochaguliwa katika nafasi ya mkutano mkuu wa CCM Taifa ni Mkuu wa wilaya ya Momba, Abiudy Saideya, Dr.Luka Siyame, Aden Mwakyonde, Zainabu Siame na Joina Siame.

Kwa nafasi za wajumbe wawili wa mkutano mkuu wa CCM mkoa, wagombea Fatuma Gingo na Yasinta Tung;ombe, walikuwa hawana upinzani baada ya kupita bila kupingwa.

Mwanaidy alisema wajumbe kumi wa halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Momba walioibuka kidedea ni Jeremia Msukwa, Benedicto Magai, Francis Simbeye na Erick Mkamba.

Wengine ni Sephania Msongole, Green Sichona, Luka Sikaponda, Leonard Simbeye na Daud Siwale.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger