Pages


BREAKING NEWS: LIVE MUDA HUU, WAANDISHI WA HABARI WA JIJI WAHAMASIKA BAADA YA MBEYA YETU BLOG PAMOJA NA BOMBA FM RADIO KUKARABATI KIPANDE CHA BARABARA BLOCK T

Chimbuko Letu | 14:04 | 0 comments

Hivi ndivyo Barabara ilivyokuwa kabla
Waandishi wa Jiji wakiwa wamefika kuwashangaa wenzao wakiwa wanafanya kazi ya kutejenga Taifa , wa pili kutoka kushoto ni Mwandishi wa Habari wa Bomba Fm Radio Richard Kamanga aliyekuwa akifanya kazi ya kutengeneza Barabara hiyo akiongea nao.
Baadhi ya wamachinga na wananchi wa eneo hilo aibu zikiwa zimewashuka na kuamua kushirikiana na Waandishi wa Habari kutoka Bomba Fm  Radio na Mbeya yetu Blog kuendelea kutengeneza njia hiyo
Waandishi wa Jiji wakiahidi kuleta kifusi kwa ajili ya kurekebisha Barabara hiyo
 Wachina wakiwa wamefika eneo la tukio na kuahidi kuwa nao wataongeza nguvu katika ujenzi wa Barabara hiyo
Mchina akipata maelekezo juu ya Barabara hiyo
Hii ndio kazi kubwa inayoendelea kufanywa na Mbeya yetu Blog sambamba na Bomba Fm Radio .

Picha na Mbeya yetu

********************
Wakati kazi ikiendelea baada ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya kuingia Mitini, na tukio hili kuripotiwa muda mchache uliopita kupitia Mtandao huu na Bomba Fm Radio huku waandishi hao wakiendelea ya kujenga Taifa ndipo Ghafla waandishi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya walipoweza kufika na kuwashangaa wenzao wakiendelea kupiga kazi na baada ya kuona aibu waliamua kuahidi kuleta kifusi kwa ajili ya matengenezo ya Barabara hiyo.

Nao Baadhi ya wamachinga wapenda maendeleo waliweza kujitokeza kwa ajili ya kuwaunga mkono waandishi wa habari walioanzisha kazi hiyo na kuwasaidia kazi inayo endelea ya ukarabati wa kipande hicho cha barabara.
Wachina nao hawakuwa mbali baada ya kusikia ripoti ya tukio hili wakaamua kufika kujionea wenyewe, na wao kuahidi kutoa mchango wao wa kuweza kutengeneza barabara hiyo.
 

Hii ndio Hali halisi ya Barabara ya Block T ambapo imeharibika na kusababisha Dala dala kutaka kugomea kupita katika Eneo hilo kuhofia kukwama.
Hii ni sinto Fahamu ambapo wakati waandishi wa Habari waliojitolea kurekebisha Barabara hiyo wakiendelea na kazi ya kuziba mashimo hayo , watumishi wa Jiji wenyewe walikuwa ndani ya Gari lao wamefunga vioo na kushangaa kinacho endelea bila kuonesha ushirikiano wowote na Baadae waliondoka, Jambo ambalo limewashangaza watu wengi, Huku wakiwa wameahidi wangerekebisha Muundombinu huo.
Mmoja ya Gari dogo likiwa limesimama baada ya kuona kuwa Njia ni mbaya 
Baadhi ya Waandishi wa Habari Kutoka Bomba Fm wakishirikiana na Mbeya yetu Blog wakianza kuchukua Kifusi na Kuziba Barabara hiyo.
Msimamizi Mkuu na Mwandishi wa Mbeya yetu Blog Joseph Mwaisango akiwa anaendelea na kazi ya kuziba eneo hilo lililoharibika
Hali halisi ya Njia hiyo
Mmoja wa wasukuma Mkokoteni akiwa amejitosa kupita katika tope na kuendelea na safari , kutokana na kwamba alikuwa hana Njia nyengine zaidi ya hiyo
Baadhi ya Waandishi wa Habari kutoka Bomba Fm Radio wakiendelea na Kazi
Kazi imepamba moto ambapo waandishi wa Habari kutoka Bomba FM wakiwa wamekomaa kuendelea kuziba mashimo katika barabara hiyo iliyo haribika kwa kiwango kikubwa huku wakazi na wafanya biashara wa eneo hilo wakiwa wanatazama bila kufanya juhudi zozote za kutengeneza, lakini wakisikia kuna mgomo wanakuwa wakwanza kwenda andamana na shughuli za kijamii kama hizi kuzisusia 
Kazi ikiwa inaendelea kwa kasi ili  kupisha Magari yaanze kutumia Njia hiyo huku Wakazi na wafanyabiashara wa eneo hilo wakiwa wanapaangalia tu, na Jiji kufika hapo na gari lao bila kufanya kitu chochote
Kazi ikiwa inaendelea kwa kasi kubwa
Kila mmoja yupo bize
Kazi inaendelea kusonga mbele Picha na Mbeya yetu
********************************
Mbeya yetu Blog kwa ushirikiano mkubwa kabisa na Bomba Fm Radio (elimisha burudisha) waamua kurekebisha kipande cha barabara inayo tumika kupitia daladala zinazo toka uyole kuelekea s/kuu kipande hicho kilichopo Block 'T'

 Ushirikiano huo wa vyombo hivyo viwili vya habari umekuja baada ya madereva wa daladala kutaka kuweka mgomo kwaajiri ya kipande hicho cha barabara kuwa kibovu kinachokuwa ni tatizo kwa daladala hizo.

Wakati tukio hilo la ukarabati  likiendelea Halimashauri ya Jiji la Mbeya wamefika na kuwashangaa tu bila hata kuchukua hatua yoyote na hatimaye kuondoka vivyo hivyo, wamachinga wa maeneo hayo pia wamegoma kutoa ushirikiano wakati wakiambiwa kuhusu masuala ya mgomo huwa mbele kwaajiri ya kuchafua amani.

Bomba Fm Radio na mbeya yetu Blog wamechukua hatua hiyo ili kuepusha migomo isiyo kuwa yalazima kutokana na kupenda amani na kuwajali watanzania ambapo Halimashauri ya Jiji ilitoa ahadi ya kutengeneza lakini mpaka sasa haijaweza kufanya jambo lolote kuhusiana na sehemu hiyo.


Mtazamo : Halimashauri ya Jiji la Mbeya mnapo wahamisha watu kutoka sehemu moja kuelekea sehemu nyingine tunaomba muhakikishe mmewawekea miundombinu ya kutosha ili kuepusha mambo machache yanayo weza kuwa ni tatizo kwa wananchi

MAMA WANNE APELEKWA KATIKA KITUO MAALUMU NA WATOTO WAKE WAWILI WALIOBAKI KWA AJILI YA UANGALIZI.

Chimbuko Letu | 08:38 | 0 comments

 
UONGOZI wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kupitia kitengo cha Ustawi wa jamii  umemtafutia kituo cha kulelea watoto wa mitaani cha Nuru Ophans Centre Mama aliyejifungua mapacha wanne na kubakia wawili baada ya kuugua Nimonia kwa ajili ya uangalizi wa karibu.
 
Hatua hiyo imekuja baada ya uongozi wa Hospitali hiyo kumfuata mama mwenye watoto hao Aida Nakawala(25) pamoja na mapacha wake waliobaki kutoka kijijini kwao Chiwanda Wilaya ya Momba mkoani hapa na kuwalaza hospitalini hapo kwa uangalizi wa karibu kwa muda wa zaidi ya wiki moja.
 
Aidha baada ya afya za watoto hao  kuimarika kwa kiwango kikubwa pia Uongozi wa Hospitali hiyo imemtafutia hifadhi katika kituo cha kulelea watoto wa mitaani cha Nuru kilichopo Uyole jijini Mbeya kwa ajili ya uangalizi wa karibu kutoka kwa wauguzi na maafisa wa ustawi wa Jamii kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mbeya.
 
Akizungumza na waandishi wa habari wakati akiwakabidhi watoto hao pamoja na mama yao kwenye uongozi wa kituo cha Nuru Orphans centre, Katibu wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, Aisha Mtanda, alisema wameguswa na mazingira anayoishi mama huyo na kuamua kumpa uangalizi kwa miezi sita zaidi.
 
Alisema jukumu hilo halipaswi kufanywa na Hospitali kwa kuwa tayari  walikuwa wamemaliza jukumu lao la kumhudumia alipokuwa ana matatizo lakini wamelazimika kubeba jukumu hilo baada ya kuguswa na mazingira na hali ya makazi ya familia hiyo.
 
Alisema Hospitali imekubaliana na uongozi wa Kituo cha Nuru kwamba apewe hifadhi mama huyo na watoto wake ili apate uangalizi wa karibu ikiwa na lengo la kunusuru maisha ya watoto waliobaki kutokana na wengine kupoteza maisha kiuzembe kwa ugonjwa wa Nimonia.
 
Aliongeza kuwa Hali ya hewa ya Mkoa wa Mbeya kwa siku zijazo kunakuwa na baridi kali sana hivyo watoto wasipokuwa kwenye uangalizi wa karibu wanaweza kupatwa na ugonjwa wa Nimonia tena kwa kukosa matunzo kama ya awali.
 
Kwa upande wake, Meneja wa Kituo cha Nuru, Amanda Fihavango alisema alikubali jukumu la kuwapokea watoto hao pamoja na mama yao kutokana na kuguswa na hali iliyowakuta ya kupotea kwa watoto wawili kati ya wanne.
 
Aliongeza kuwa ingawa anakabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo za kiuchumi atajitahidi kwahudumia kadri ya uwezo wake na kuomba wasamaria wema watakaoguswa na jambo hilo kujitolea kwa hali na mali kufanikisha kuokoa uhai wa watoto hao pamoja na wengine anaowalea.
 
Alisema kituo chake hupokea watoto waliookotwa baada ya kutupwa na wazazi wao au mama zao kufariki mara baada ya kutoka kujifungua ambao hupelekwa na Serikali kupitia Ustawi wa Jamii ingawa haichangii fedha zozote baada ya kuwapeleka.
 
Mtu yoyote mwenye kuguswa anaweza kuwasilisha mchango wake kituoni hapo au kuwasiliana na Meneja wa Kituo cha Nuru kupitia namba za Simu  0754 043004 kwa ajili ya kusaidia watoto hao pamoja na mama yao kuishi hapo kwa muda wa miezi sita.
 

TIMBWILI LAZUKA BAADA YA VIONGOZI WA SERIKALI KULA PESA ZA WANACHI.

Chimbuko Letu | 01:17 | 0 comments

Mwenyekiti wa Mtaa wa Mapelele kata ya Ilemi, jijini Mbeya anashtumiwa kwa kutafuna pesa shilingi 1,300,000 zilizochangwa na wananchi kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya serikali ya mtaa.

Bofya hapa kusikiliza habari kamili inayoletwa kwako na mwandishi wetu Greyson Salufu Chatanda.


MTENDAJI WA KIJIJI NA HALMASHAURI YA KIJIJI WATIMULIWA KIJIJI CHA IWIJI KWA UFUJAJI WA MBOLEA ZA RUZUKU

Chimbuko Letu | 07:27 | 0 comments
Kushoto Afisa tarafa Aaron Sote akipokea funguo toka kwa mtendaji Anton Ndisa 

Afisa Kilimo wilaya Marselin Mlelwa atitoa takwimu  za mgao wa mbolea iliyotolewa Octoba 10 mwaka jana kwa kijiji hicho baada ya kupitishwa na Kamati ya Mbolea ya Wilaya ambayo mwenyekiti wake ni Mkuu wa Wilaya.

Wananchi wakifuatilia mkutano huo kwa makini


Saimoni Kasebele moja kati ya wajumbe kamati ya mbolea ambayo haikufanya kazi kijijini

Moja kati ya wananchi ambao waliwekwa mahabusu na mtendaji baada ya kufuatilia mgao wa mbolea


Wajumbe waliotimuliwa


Mbolea inayosadikiwa kuibwa 



Kwa picha zaidi tazama hapa PICHA ZAIDI
Wananchi wa kijiji cha Iwiji Kata ya Iwiji wilaya ya Mbeya wamemtimua Mtendaji wa Kijiji hicho ambaye pia ni Kaimu Mtendaji Kata aliyefahamika kwa jina la Anthon Ndisa kwa tuhuma za ubadhilifu wa Mbolea za ruzuku mifuko 189 iliyotolewa na serikali kwa kipindi cha msimu wa 2013/2014.

Hatua hiyo imechukuliwa na wananchi hao katika mkutatano wa hadhara uliofanyika kijijni hapo ambapo Afisa Kilimo wilaya Marselin Mlelwa atitoa takwimu  za mgao wa mbolea iliyotolewa Octoba 10 mwaka jana kwa kijiji hicho baada ya kupitishwa na Kamati ya Mbolea ya Wilaya ambayo mwenyekiti wake ni Mkuu wa Wilaya.

Afisa Tarafa ya Isangati Aaron Sote ambaye alimwakilisha Mkuu wa Wilaya ndiye alisimamia mkutano huo amesema kuwa Afisa kilimo ndiye mwenye jukumu la kutoa taarifa ya mgao wa mbolea kama kamati ilivyopitisha.

Baada ya kufunguliwa mkutano  na Mwenyekiti wa kijiji Patson Ngao Afisa Tarafa alimkaribisha Afisa Kilimo kusoma jinsi mgao wa mbolea ulivyokwenda ambapo alisema Kitongoji cha Mabula kilipata mbolea ya Dap mifuko 20 Urea 20, Kitongoji cha Iwiji Dap mifuko 8 Urea 20,Kitongoji cha Soweto mifuko 6 Dap na Urea mifuko 16.

Kitongoji cha Magole kilipata Dap mifuko 6 na Urea mifuko 16,Kitongojo cha Mtukula Dap mifuko 6 na Urea mifuko 16 wakati Kitongoji cha Ntinga kilipata Dap mifuko 8 na Urea mifuko 20 wakati Kitongoji cha Vimetu kikipata Dap mifuko 7 na Urea mifuko 20.

Katika mgao huo kulikuwa na upungufu wa mifuko 50 ya Dap na Urea mifuko 36 ambayo wakulima hawajapatiwa na kwamba ikifika wananchi wagawiwe ili kukamilisha idadi ya mifuko 189 kwani hivi sasa mifuko iliyogawiwa ni mifuko 139 tu.

Baada ya kusomwa taarifa hiyo wananchi walitaharuki wakidai kuwa hesabu hizo zimetengezwa na Mtendaji Anthon Ndisa kwa manufaa yake kwani wananchi hawajapata mbolea hiyo licha ya kutoa taarifa kwa uongozi wa Wilaya kupitia Afisa Pembejeo Lupakisyo Masuba.

Kutokana na kutoridhishwa na taarifa hiyo na kwamba wananchi wamehujumiwa na uongozi wa kijiji kupitia viongozi wa vitongoji ambao walikiri kupokea mbolea hiyo na kuigawa wakati kuna kamati mbolea ya kijiji ambayo ndiyo ilikuwa na jukumu la kugawa ambapo uongozi wa kijiji ukidai kamati hiyo ilivunjwa.

Mmoja wa wajumbe wa Kamati ya pembejeo Simon Kasebele amesema kuwa kati iliyokuwa na wajumbe sita ambao ni Mwenyekit Venance Lwinga,Lucia Mose,Sara Kasalama,Patson Kayelewe na Eva Makanika haikufanya kazi kutokana na agizo la Mtendaji aliyedai kuwa kamati imevunjwa wakati siyo kweli bali ilikuwa ni njama za kuwahujumu wananchi kwa manufaa yao.

Baada ya majadiliano marefu wananchi waliamua kuirudisha Kamati ya Mbolea huku wakimtaka Mtendaji kuondolewa haraka ili kuepusha ufujwaji wa mali za kijiji na kuwatimua wenyeviti wote wa vitongoji na kumwacha Mwenyekiti wa kijiji pekee Patson Ngao wakidai hahusiki na ubadhilifu kwani alizungukwa na Mtendaji kupitia wenyeviti wa vitongoji.

Kwa upande wake Afisa Kilimo Marselin Mlelwa amesema taarifa ataifikisha kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ili kutoa maamuzi kwa vile Mtendaji ni Mwajiriwa hivyo lazima taratibu za utumishi lazima zifuatwe.

Ili kuhakikisha hakuna nyaraka zozote zinachukuliwa Ofisi Mwenyekiti na Kamati ya Mbolea watafanyia shughuli zao katika ghala la Kijiji wakati Mtendaji aliagizwa kubaki na funguo hadi hapo Halmashauri itakapotoa taarifa zake baada ya ukaguzi.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Upendo Sanga amekiri kupokea taafa za malamiko ya wananchi wa Iwiji na kuwataka kuwa na subira kwani serikali ina utaratibu wake ambao lazima ufuatwe pindi mtumishi anapotuhumiwa kwa jambo lolote ikiwa na pamoja na kuunda Tume ya Uchunguzi na Wakaguzi ili kupata Ushahidi.

Uchunguzi uliofanywa baada wananchi kulalamikia utaratibu uliotumika kugawa mbolea hiyo Mtendaji wa Kijiji alirejesha mifuko 50 ya Dap ambayo imehifadhiwa kwa mmoja wa Mawakala kijijini hapo ili kuficha ushahidi na kuonekana mbolea hiyo ilikuwepo wakat ukweli ni kwamba mbolea hiyo tangu itolewe mwezi Octoba wananchi hatanufaika nayo kwa kuwa msimu wa kilimo umepita na kijiji kukabiliwa na hatari ya njaa.

Mbali ya tuhuma ya Mbolea Mtendaji anatuhumiwa kufuja fedha za serikali na michango ya wananchi kwa ajili ya kituo cha Afya hivyo wamemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri anapofanya uchunguzi wa Mbolea afanye ukaguzi pia mradi wa Kituo cha Afya na kama ikibainika Mtendaji na Halmashauri ya Kijiji wafikishwe kwenye vyombo vya sheria.

Na Ezekiel Kamanga

Tuzo ya mwalimu bora duniani yazinduliwa

Chimbuko Letu | 23:17 | 0 comments


Mwenyekiti wa Wakfu huo Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton.
Baadhi ya walimu jijini Mbeya  wameipokea kwa mtazamo tofauti  juu ya kuzinduliwa kwa tuzo ya mwalimu duniani, atakaye thibitisha kuwa mchango wake kwa jamii umekuwa bora zaidi na kujishindia shilingi bilioni 1 na milioni 650.



KWA HABARI KAMILI INALETWA KWAKO NA GREYSON SALUFU...... Bofya hapa chini kwa habari kamili.

WANYANYASAJI WA WATOTO WAANZA KUCHUKULIWA HATUA MKOANI MBEYA.

Chimbuko Letu | 07:40 | 0 comments



JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia mwanamke mmoja Mwanahawa Nasoro(32) Mkazi wa Mtaa wa Airport Kata ya Iyela Jijini Mbeya akituhumiwa kumfanyia vitendo vya unyanyasasaji Mtoto wa ndugu yake.
 
Mwanamke huyo anatuhumiwa kumtesa, mtoto John Msumba(3) ambaye ni Shangazi yake baada ya kumfungia ndani kumnyima chakula na kumpa kipigo kikali kilichompelekea kuwa na majeraha mwilini mwake pamoja na maumivu makali yaliyosabisha kulazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kwa matibabu zaidi.
 
Akizungumza na Mtandao huu, Mjumbe wa Mtaa wa Airport, Rehema Mohammed alisema kuteswa na kukamatwa kwa Mwanamke huyo kuligundulika Machi 12, Mwaka huu majira ya saa nne asubuhi kufuatia kuwepo kwa msiba jirani na nyumba yake.
 
Alisema wakati watu wako msibani na mlango wa nyumba ya Mwanamke huyo ukiwa umefungwa na kufuli kwa nje ilisikika sauti ya Mtoto akilia ndani jambo ambalo liliwashangaza wengi ndipo alipotoa taarifa kwa Mwenyekiti wa Mtaa Enock Mwampagama ambaye pia alitoa taarifa kwa Mtendaji wa Mtaa aliyelitaarifu Jeshi la Polisi.
 
Alisema baada ya Mwanamke huyo kubanwa alikiri kuwepo kwa Mtoto ndani na kwamba alikuwa akimfanyia hivyo kutokana na tabia yake ya kujisaidia haja kubwa hovyo hali iliyokuwa imemchosha na kuamua kumpa adhabu kama hiyo.
 
Alipoulizwa kuhusiana na wazazi wa Mtoto huyo alidai kuwa hafahamu mahali alipo mama mzazi na kuongeza kuwa baba yake aliyefahamika kwa jina la Sumba Dinda kuwa yupo machimboni Wilayani Chunya kwenye Migodi ya Dhahabu.
 
Jeshi la Polisi limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa Mwanamke huyo anashikiliwa hadi hapo Afya ya mtoto ambaye ni mhanga wa Tukio hilo itakapoimarika ndipo atakapofikishwa mahakamani kujibu mashtaka yanayomkabili.
 
Wakati huo huo baadhi ya Wasamaria wema wameziomba taasisi zinazoshughulikia masuala ya unyanyasaji wa kijinsia na watoto zikiwemo Mtandao wa Waandishi wa habari Wanawake na Jinsia (TAMWA) na Taasisi ya Jinsia (TGNP) kuingilia kati maswala hayo ili kukomesha vitendo hivyo katika jamii.
 
Aidha baadhi ya wasamaria wema wajitokeza kuchangia fedha za matibabu ya mtoto huyo yanayoendelea katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya baada ya mmoja wa Waandishi wa Mtandao huu ambaye pia ni Mtangazaji wa Kituo cha Redio cha Bomba cha Jijini Mbeya kuendesha harambee fupi katika kipindi chake na kufanikiwa kukusanya shilingi 35,000/= zilizotumika kununulia madawa.
 
Mbali na hilo TAMWA inaombwa kushughulika moja kwa moja na mtoto huyo ili kuhakikisha haki inapatikana ikiwa ni pamoja na kupiga vita unyanyasaji wa kijinsia uliokithiri ndani ya jamii kutokana na juhudi ziliooneshwa na mtandao huo katika kukabiliana na hali hiyo kwa kutoa Elimu kwa wanahabari mara kwa mara katika kuibua vitendo hivyo na kuvikemea.


Na Ezekiel Kamanga.

WATOTO WAWILI KATI YA MAPACHA WANNE WAMEFARIKI DUNIA, RAMBIRAMBI KUTOKA USWISI ZAPOKELEWA KIJIJINI KWAO.

Chimbuko Letu | 07:26 | 0 comments

Jeneza likiwa na mwili wa Marehemu tayari kwa Ibada ya Mazishi iliyofanyikia Nyumbani kwao Chiwanda.

Mchungaji wa Kanisa la Africa Mission Church wanakosali wazazi wa Marehemu akiongoza ibada ya Mazishi.

baadhi ya Waombolezaji wakielekea Makaburini.

Joseph Mwaisango akiwa amebeba Jeneza lenye mwili ya marehemu kuelekea Makaburini tayari kwa safari ya mwisho


Mchungaji akisoma neno la Mungu kutoka kwenye Biblia lenye ujumbe kwa Waombolezaji na wafiwa ambapo alisema hata kama alikuwa ni mtoto mchanga alikuwa akivuta pumzi kama sisi hivyo naye amepaswa kupewa heshima zote kama binadamu.

Mwili wa Marehemu ukishushwa kaburini.

Kaburi likifukiwa baada kukamilika kwa taratibu zote ambapo mwili wa marehemu ulizikwa katika makaburi ya Kijiji wanakozikwa Wananchi wengine.

Kwa mujibu wa mila za kabila la Wanyamwanga vijana hawa walikuwa wakisiliba kaburi baada ya kumaliza mazishi.

Ezekiel Richard Kamanga ambaye ni mwandishi wa Habari kutoka redio ya Bomba fm ya Jijini Mbeya akizungumza machache kwa wafiwa na wanakijiji kwa niaba ya Wanahabari wenzao ambao hawapo pichani Venance Matinya wa gazeti la JamboLeo na Joseph Mwaisango wa mbeya yetu blog




KATIKA hali ya kusikitisha Watoto wawili kati ya Wanne ambao ni mapacha waliozaliwa kwa pamoja na mwanamke Aida Nakawala Mkazi wa Kijiji cha Chiwanda Wilaya ya Momba Mkoani Mbeya wamefariki dunia kwa ugonjwa wa Nimonia.

Watoto hao wamefariki kwa mida tofauti ambapo Mtoto wa Kwanza alifariki Nyumbani kwao baada ya kuugua ghafla ndipo hali za wengine zilipoanza kutia shaka na kulazimu Waandishi wa Habari wa Mtandao wa Mbeya Yetu, Gazeti la Jambo Leo na Redio ya Bomba Fm waliohudhuria mazishi ya Mtoto huyo kulazimika kuwakimbiza katika Hospitali ya Wazazi Meta kwa matibabu zaidi.

Hata hivyo baada ya kupokelewa kwa watoto hao Watatu mtoto mmoja aliaga dunia baada ya kuchelewa kupata matibabu kutokana na kubanwa na kifua na kusababisha kushindwa kupumua vizuri.

Hali za watoto wawili waliobaki wanaendelea vizuri na matibabu na kwa mujibu wa Daktari anayewatibu amesema taratibu za Hospitali hiyo ni kupokea watoto waliochini ya Miezi miwili lakini hao wamezidi umri huo hivyo badala ya kupelekwa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya wataendelea kuwepo Meta hadi hapo hali zao zitakapoimarika.

Baadhi ya wananchi na wauguzi katika Hospitali ya Wazazi Meta wamesema sababu ya watoto hao kuugua ni kutokana na  kukosekana kwa uangalifu wa karibu katika malezi ya watoto hao ukilinganisha na maisha ya vijijini kukosa watu wenye uelewa wa afya za watoto.

Wengine wameitupia lawama moja kwa moja Serikali kwa kushindwa kuchukua hatua za haraka tangu watoto walipozaliwa ili kujiridhisha na mazingira wanayopaswa watoto hao kuishi kwa kuwapatia msaada wa karibu na ushauri wa kitaalamu.

Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Mbeya, Thobias Mwalwego, alikiri kuwepo kwa urasimu katika Idara yao kwa madai kuwa tangu watoto hao walipokuwa wamezaliwa walipata taarifa na kuchukua hatua kwa afisa mmoja kufika kijijini na kuchukua picha zao.

Alisema urasimu unakuja kutokana na Ofisi ya Wilaya na Mkoa kukosa fungu la dharula ambapo barua za maombi zote hupelekwa makao makuu kwa Kamishna wa Ustawi wa Jamii ambapo Ofisi yake huchukua muda mrefu kurudisha majibu kutokana na waombaji kuwa wengi.

Alisema kila ofisi katika Ngazi ya Mkoa ingekuwa na fungu la Dharula kama ilivyo katika Ofisi zingine hali ambayo ingeweza kusaidia kuepusha vifo vya watoto hao kutokana na kupatiwa msaada wa ushauri na makazi rafiki kwa malezi ya mapacha wanaozidi wawili.

Aidha alishauri kila Halmashauri Nchini kutenga bajeti za kusaidia majanga kama hayo na vitu vya dharula wakati Serikali inajipanga kutekeleza kutokana na taratibu zake kuchukua muda mrefu ili kuweza kukabiliana na hali yoyote na muda muafaka.
 Meneja wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) Kanda ya Nyanda za Juu kusini, Ahmed Issa katikati na Joseph Mwaisango wa Mbeya yetu Blog wakimkabidhi Aida Nakawala msaada wa pesa kiasi cha shilingi laki tano 500,000/ toka wa watanzania waishio nchini Uswisi

Baadhi ya watumishi wa  Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) Kanda ya Nyanda za Juu kusini wakiwa wamewabeba watoto hao

Joseph Mwaisango alipokwenda kuwatembelea Hospitali ya wazazi Meta watoto wawili waliobakia na hali zao kwa sasa zinaendelea vizuri
Wakati huo huo Umoja wa  Watanzania waishio nchini Uswisi (TAS) wametoa msaada wa Fedha taslimu shilingi Laki tano(500,000/=) kwa mama Aida Nakawala kwa ajili ya kusaidia kulea watoto wengine waliobaki.

Akikabidhi msaada huyo kwa mama huyo kijijini kwao Chiwanda Wilayani Momba, Meneja wa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) Kanda ya Nyanda za Juu kusini, Ahmed Issa kwa niaba ya Watanzania hao alisema wameguswa sana na hali hiyo na kuahidi kuendelea kuchangia kila mara.

Aidha alisifu utendaji kazi wa Waandishi wa Habari hususani Mbeya yetu Blogwaliofanikisha kuibua jambo hilo na kulitolea taarifa kila wakati jambo lililosaidia kufahamisha watu wengi wakiwemo wanaoishi nje ya Tanzania na kutuma kile wanachokuwa wameguswa nacho.

Mbali na Hilo, Meneja wa TMA Kanda ya Mbeya, Ahmed Issa, pia amejitolea kuusafirisha mwili wa Marehemu kutoka Hospitali ya Meta Mbeya hadi Kijijini kwao Chiwanda Wilayani Momba kwa ajili ya taratibu za Mazishi.

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger