Pages


Home » » KUPASUKA KWA KEBO YA KUSAMBAZIA UMEME, SAI JIJINI MBEYA NDIO CHANZO CHA MKOA KUWAGIZA.

KUPASUKA KWA KEBO YA KUSAMBAZIA UMEME, SAI JIJINI MBEYA NDIO CHANZO CHA MKOA KUWAGIZA.

Kamanga na Matukio | 04:52 | 0 comments
Na mwandishi wetu
Imeelezwa kwamba tatizo la umeme linaloyakabili baadhi ya maeneo mkoani Mbeya kuwa chanzo chake ni kupasuka kwa kebo inayosambaza umeme kutoka Sai eneo la mwakibete kwenda Iyunga.

Akiongea na mwandishi wetu ofisini kwake meneja wa TANESCO Injinia Kyando amesema kuwa tatizo hilo limeshapatiwa ufumbuzi na hadi sasa wanaendelea na marekebisho eneo la Iyunga na kwamba mpaka kufikia  jioni ya leo zoezi hilo litakuwa limekamilika.

Ameongeza kuwa kutokana na matengenezo yanayoendelea umeme utakatwa siku nzima ili kuepukana na hatari ambayo inaweza kutokea kwa wananchi na kusababisha athari.

Aidha amewaomba radhi wananchi mkoani hapa kwa usumbufu utakaojitokeza kutokana na marekebisho hayo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger