AJALI YAUA MMOJA NA MAJERUHI 17 WALAZWA WILAYANI RUNGWE

Kamanga na Matukio | 04:04 | 0 comments
GARI YA AINA YA COSTA T 399 AUD ILIYOGONGWA KWA NYUMA NA KISHA KUPINDUKA ENEO LA KANYEGELE UWANJA WA NDEGE WILAYANI RUNGWE

HUU NI UPANDE WA NYUMA WA COSTA HIYO 


BAADHI YA WASIO WASAMARIA WEMA WAKITAFUTA FEDHA ZILIZODONDOKA KUTOKA KATIKA BASI HILO HATA HIVYO VIJANA HAO WALIZOMEWA NA WANANCHI WALIOFIKA KUTOA MSAADA


HILI NDILO ROLI LILILO IGONGA COSTA KWA NYUMBA NA KUSABABISHA AJALI HIYO NAMBARI YA ROLI T 712 CZC NA TERA LENYE NAMBALI T 444 CCZ LIKIWA NA SHEHENA YA MBOLEA


MOJA KATI YA MAJERUHI AKIWA KATIKA HOSPITALI YA TUKUYU

BAADHI YA MAJERUHI WAKISUBIRI HUDUMA


BAADHI YA NDUGU WAKISUBIRIA KUWAONA NDUGU ZAO WALIOPATA AJALI

BAADHI YA WAGONJWA WAKISAFIRISHWA KWENDA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA



KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WILAYA YA RUNGWE ILIPOTEMBELEA MAJERUHI WALIOPATA AJALI




                                                                             

                     Picha na  Ezekiel Kamanga 

AJALI MBAYA IMETOKEA MBALIZI MBEYA MMOJA AFARIKI PAPO HAPO NA WANNE MAJERUHI

Kamanga na Matukio | 04:01 | 0 comments

MAREHEMU SELEMANI JUMA SELEMANI ALIYEKUWA TINGO WA ROLI HILO AMEFARIKI PAPO HAPO 


AJALI HII IMETOKEA KWENYE MTEREMKO WA MBALIZI ROLI HILO INA SEMKANA LILI FERI BREKI







Magufuli akumbwa na kashfa nzito!

Kamanga na Matukio | 04:00 | 0 comments

Hii imetoka kwenye hotuba ya kambi ya upinzani. Sehemu hii inaonyesha ubadhirifu wa fedha kwenye wizara iliyoko chini ya Dr John Pombe Magufuli.
Mheshimiwa Spika, baada ya fedha hizi kupunguzwa kiasi cha shilingi bilioni 95 na kupelekwa wizara ya uchukuzi zilibakia kiasi cha shilingi bilioni 252.975 katika kifungu hiki, leo tumelazimika kulikumbusha Bunge kuhusiana na suala hili kwani kwa mujibu wa ripoti ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali ya mwaka husika wa fedha kuhusiana na kifungu hiki alisema, naomba kunukuu “malipo ya madeni ya mwaka wa nyuma yaliyolipwa kwa fedha za 2011/2012 kwa kutumia jina la mradi usio halisi Tshs. 252,975,000,000.

Miradi katika wizara ilipewa namba 4168 kwa ajili ya kupitisha malipo ya madeni ya miaka ya nyuma kwa miradi inayotekelezwa na TANROADS. Namba hii sio halisi” (chanzo: taarifa ya CAG uk.160,fungu 98)

Mheshimiwa Spika, fedha hizi “zilizopotea”au “kulipwa kifungu hewa” ni sawa na fedha zote zilizotengwa kwa ajili ya barabara ifuatazo kwa mwaka huu wa fedha 2013/2014;

i. Barabara
ya Usagara-Geita-Kyamyorwa
(KM 422)

ii. Barabara
ya Kigoma-Kidahwe-Uvinza-
Kaliua-Tabora (KM 443)

iii. Barabara
ya Nangurukuru-Mbwemkulu
(KM 95)

iv. Barabara
ya Sumbawanga-Matai-Kasanga
Port (KM 112)

v. Barabara
ya Manyoni-Itigi-Tabora (KM264)

vi. Barabara
ya Tabora-Ipole-Konga-Mpanda
(KM 359)

vii. Barabara
ya Kidatu-Ifakara-Lupilo-Malinyi-
Londo-Lumecha/Songea(KM-396)

viii. Kuondoa
msongamano barabara za Dar
(KM-102.15)

Aidha, ni sawa na kusema kuwa barabara ya lami yenye urefu wa kilomita 316.218 imepotea kwa kutumia mahesabu ya wizara ya ujenzi kuwa kilomita moja ya lami inajengwa kwa kiasi cha shilingi milioni mia nane (800,000,000), hii ni sawa na kusema kuwa barabara ya kutoka Manyoni-Itigi-Tabora (KM 264) Changanya na barabara ya kutoka Chunya – Makongorosi (KM 43) na Barabara ya Tangi Bovu –Goba (KM 9), zimepotea kutokana na ufisadi huu.

Chanzo: Hotuba ya kambi rasmi ya upinzani bungeni
Soma hapa zaidi>>> Jamii Forums

Wananchi Mkoani Mbeya wamelipongeza Jeshi la Polisi.

Kamanga na Matukio | 04:05 | 0 comments
Meneja wa Benki ya NMB kanda ya nyanda za juu kusini Bi.Lucresia Makirie akimkabidhi pikipiki tatu

Mwenyekiti wa kikosi cha Mafanikio cha kuchangisha fedha na michango ya kuliwezesha Jeshi la Polisi kufanya kazi katika Mazingira mazuri, Julius Kaijage

Mwenyekiti wa kikosi cha Mafanikio Julius Kaijage akimkabidhi pikipiki mbili na matairi 4 ya gari pamoja na mabati mkuu wa mkoa wa Mbeya Abas Kandoro vifaa hivyo vyote vimetoka kwa wadau wa ulinzi mkoani hapa




Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akiongea na wadau mbali mbali kwenye hafla fupi ya kupokea misaada toka kwa wadau wa ulinzi mkoani hapa

Mwenyekiti wa kikosi cha Mafanikio cha kuchangisha fedha na michango ya kuliwezesha Jeshi la Polisi kufanya kazi katika Mazingira mazuri, Julius Kaijage amesema Askari wa Jeshi la Polisi wanafanya kazi katika mazingira magumu hivyo ni jukumu la kila mwananchi kuhakikisha analiwezesha kwa hali na mali.

Meneja wa Benki ya NMB kanda ya nyanda za juu kusini Bi.Lucresia Makirie amesema benki yake imetoa msaada Pikipiki tatu kusaidia jeshi hilo ili zisaidie katika ulinzi shirikishi katika mkoa wa Mbeya


Kamanada wa Polisi Mkoani Mbeya Diwani Athumani amewapongeza wadau mbalimbali waliojitokeza kulisaidia jeshi hilo ambapo amewahahakikishia wananchi wa mkoa huu kuwa kwa sasa mkoa wa mbeya upo katika mazingira salama kutokana na ushirikiano uliopo kati ya wananchi na jeshi hilo .













Picha ya pamoja
BAADHI ya Wananchi Mkoani Mbeya wamelipongeza Jeshi la Polisi Mkoani hapa kwa kuendelea kusambaratisha na kumaliza kabisa mtandao wa ujambazi kutokana na majambazi wengi  kukamatwa na wengine kuawa.
  
Pongezi hizo zimekuja Siku moja baada ya Jeshi hilo kuwauwa watu watano wanaosadikiwa kuwa ni majambazi katika majibizano ya kurushiana risasi kati ya Askari na majambazi hayo katika tukio lililotokea katika kijiji cha Garijembe Wilaya ya Mbeya.
  
Katika kuhakikisha Jeshi hilo linaendelea  kufanya kazi katika mazingira mazuri na kwa mafanikio  na kuunga mkono juhudi zao, Wadau mbali mbali  leo  wamejitokeza kulichangia jeshi hilo katika Hafla iliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoani hapa.
  
Hafla hiyo ambayo mgeni rasmi alikuwa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro Jumla ya Shilingi Milioni 28 zilipatikana vikiwemo vifaa mbali mbali.
  
Mwenyekiti wa kikosi cha Mafanikio cha kuchangisha fedha na michango ya kuliwezesha Jeshi la Polisi kufanya kazi katika Mazingira mazuri, Julius Kaijage amesema Askari wa Jeshi la Polisi wanafanya kazi katika mazingira magumu hivyo ni jukumu la kila mwananchi kuhakikisha analiwezesha kwa hali na mali.
  
Katika Hafla hiyo Jumla ya Pikipiki tano zilinunuliwa ambapo kati ya hizo Tatu zimetolewa na Benki ya Nmb kwa thamani ya Shilingi Milion 5.4, wakati kamati ikinunua pikipiki Mbili kwa Thamani ya Shilingi Milioni Moja na Laki Nane.
  
Mbali na michango hiyo pia Wakala wa Majengo mkoa wa Mbeya (TBA) imetoa mabati 22 ya Geji 28 yenye thamani ya Shilingi 460,000/=, pia kamati ya Mafanikio imenunua Matairi nane yenye thamani ya Shilingi Milioni 3,020,000/=,pamoja na mafuta kwa ajili ya magari ambayo ni Lita 360 kwa Mwaka zilizoahidiwa na kampuni ya G4S.
  
Mbali na pongezi hizo Wananchi hao wamemshauri Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani mbali na kupambana na uhalifu katika Mkoa wa Mbeya na kuwasisitiza watu wanaofanya shughuli zisizokuwa na uhalali kuacha mara moja au kuhama Mkoa pia wapendekeza kufanya ziara za kushtukiza katika Vituo vidogo vya Polisi.

Kwa upande wake Kamanada wa Polisi Mkoani hapa Diwani Athumani amewapongeza wadau mbalimbali waliojitokeza kulisaidia jeshi hilo ambapo amewahahakikishia wananchi wa mkoa huu kuwa kwa sasa mkoa wa mbeya upo katika mazingira salama kutokana na ushirikiano uliopo kati ya wananchi na jeshi hilo .

Na Ezekiel Kamanga,Mbeya,
 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger