Pages


Home » » WATU WAWILI WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA KWA TUHUMA ZA KUKUTWA NA MADAWA YA KULEVYA NA NOTI BANDIA

WATU WAWILI WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA KWA TUHUMA ZA KUKUTWA NA MADAWA YA KULEVYA NA NOTI BANDIA

Kamanga na Matukio | 05:52 | 0 comments

Kamanda wa Jeshila Polisi mkoani Mbeya Advocate Nyombi
*****
Na mwandishi wetu
Jeshi la polisi mkoa wa Mbeya linawashikilia watu wawili wakazi wa Tunduma na Kyela baada ya kukutwa na dawa za kulevya aina ya Kokeini na Bangi pamoja noti 3 za bandia za  shilingi elfu kumi.

Akiongea na waandishi wa habari kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Anecletusi Malindisa amesema kuwa jana majira ya saa 6 za mchana Imani Chaula mwenye umri wa miaka 23 mkazi wa Mwaka Tunduma alikutwa na kete 50 za bangi akiwa anauza.

Aidha amemtaja mtuhumiwa mwingine kuwa ni Ramadhani Abasi mwenye umri wa miaka 29 mkazi wa Kyela kati ambaye alikuwa na kete kumi za dawa ya kulevya aina ya Kokeini na noti 3 bandia za elfu kumi.

Amesema mtuhumiwa huyo ni muuzaji wa dawa za kulevya na kwamba watuhumiwa wote wamefikishwa leo mahakamani kosomewa mashtaka yao.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger