Pages


Home » » MTOTO AFARIKI BAADA YA KUSHAMBULIWA NA KUNDI LA NYUKI.

MTOTO AFARIKI BAADA YA KUSHAMBULIWA NA KUNDI LA NYUKI.

Kamanga na Matukio | 03:35 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbozi.
Mtoto Runi Fabi(5) mkazi wa Kitongoji cha Namleya,Ilembo,Kata ya Vwawa,Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya amefariki dunia baada ya kushambuliwa na kung'atwa na kundi la nyuki.

Tukio hilo limetokea Mei 27 mwaka huu majira ya saa sita mchana,wakati akicheza na watoto wenzake nje kidogo ya nyumba yao.

Balozi wa mtaa huo Bwana Hanzi Wega, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kubainisha ya kwamba tukio hilo ni la pili kutokea mtaani kwake.

Ameongeza kuwa mwezi Mei mwaka jana mwanamke marehemu Namyugumbi Nzunda, aliuawa baada ya kuvamiwa na kundi la nyuki.

Hata hivyo Baba mzazi wa mtoto huyo Bwana Fabi Mjewa amesema alishangaa kuletewa mwanae akiwa amezirai lakini alipopelekwa Hospitali ya Wilaya ya Mbozi, aliambiwa mwanae kashafariki na hivyo mazishi yake kufanyika Mei 28 mwaka huu katika mtaa wa Ilembo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger