Pages


Home » » MTOTO AFA MAJI AKIJARIBU KUOKOA KANDAMBILI/YEBOYEBO.

MTOTO AFA MAJI AKIJARIBU KUOKOA KANDAMBILI/YEBOYEBO.

Kamanga na Matukio | 05:08 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Mkazi wa Kitongoji cha Mwanjelwa, Kijiji cha Itaka, Kata ya Itaka, Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya Daniel Bahati Mgala (3) amefariki dunia katika kisima cha maji ya kufyatulia matofali.

Tukio hili limetokea kijijini hapo Mei 23 mwaka huu majira ya saa nne asubuhi wakati marehemu akiwa na mwenzake alikuwa akiifuata Yeboyebo moja iliyotupwa na mwenzie katika kisima hicho alipojaribu kuifuata alizama na kufa papo hapo baada ya kunywa maji hayo.

Aidha mwenzake alipoona kazama alimwita mzazi Bahati Mgala na alipofika alikuta mwanae amekwishafariki ndipo alitoa kwa Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho Bwana Nsinkini na Mwenyekiti Bwana Mwashilindi.

Viongozi hao baada ya kupewa taarifa hizo moja kwa moja walizifikisha katika Kituo cha Polisi, ambapo askari wa jeshi hilo walifika na Daktari wa Zahanati ya Nambizo Bwana Mtambo na kuthibitisha kifo hicho cha mtoto huo.

Mara baada ya kukamilika uchunguzi mwili wa marehemu ulikabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya maziko ambapo maziko yalifanyika katika makaburi ya Kijiji cha Shitungulu, Wilaya ya Mbozi majira ya saa tano asubuhi.

Hata hivyo Kamanda wa Polisi mkoani hapa Advocate Nyombi amethibitisha kutokea kwa tukio hili na kwamba uchunguzi wa tukio hili unaendelea.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger