Pages


Home » » WATU WATATU WASHTAKIWA KWA KUJERUHI.

WATU WATATU WASHTAKIWA KWA KUJERUHI.

Kamanga na Matukio | 03:34 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Watu watatu wakazi wa Tuduma Kati, Wilaya mpya ya Momba, Mkoani Mbeya wameshtakiwa kwa tuhuma za kujeruhi.

Watuhumiwa hao ni pamoja na Martha Ndabila(30),Gibe Prosper(37) na Victor Haonga(37) ambapo wote kwa pamoja walifikishwa katika Mahakama ya mwanzo Tunduma Mei 29 mwaka huu.

Watuhumiwa hao walifikishwa mbele ya Hakimu Leonard Kazimzuri wa mahakama hiyo, wakidaiwa kumjeruhi Bwana Elias Cheyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mamlaka ya Halmashauri ya mji mdogo wa Tunduma, Mei 28 mwaka huu majira ya saa 5:30 asubuhi.

Akisoma mashtaka mbele ya mahakama hiyo PP Nathani amesema kuwa watu hai wametenda kosa la jinai kifungu cha 241 sura ya 16 ya marekebisho ya sheria ya nchi ambapo kesi hiyo imesajiliwa kwa namba ya 236 ya mwaka 2012.

Baada ya kusomewa shtaka hilo watuhumiwa walikana kutenda kosa hilo na kesi hiyo kupigwa kalenda mpaka June 11 mwaka huu,na Hakimu kuweka bayana dhamana kwa washtakiwa kuwa na wadhamini wawili kila mmoja ambapo wote walidhaminiwa.

Aidha sababu za wananchi hao na kufikishwa mahakamani ni kutokana na kutokubaliana na taarifa ya mapato na matumizi iliyosomwa katika mkutano wa mtaa,ambapo wananchi hao hawakutaka kukubaliana na taarifa ya Mwenyekiti huyo wa halmashauri  wakidai si sahihi na kwamba amefuja pesa za wananchi zaidi ya shilingi milioni 2.5.

Kufuati hali hiyo walimtaka mwenyekiti huyo Bwana Cheyo kujiuzuru kwa kutia saini kwenye karatasi jambo ambalo kiongozi huyo alilikataa na kuuvunja mkutano majira ya saa 6:30 mchana na wananchi kutawanyika.

Sakata hilo halikuishia hapo majira ya saa 5:00 usiku, Jeshi la polisi liliwakamata watuhumiwa hao kwa mahojiano katika Kituo cha Polisi Tunduma, hali iliyowatia hasira wananchi hao na kusababisha taflani kituoni hapo  baada ya wananchi wengine kutaka kuvamia ili kuwatoa watuhumiwa.

Hata hivyo baada ya kuona mambo yanazidi kuwa magumu Jeshi la Polisi Mei 29 mwaka huu majira ya saa nne asubuhi, lililazimika kuandaa hati ya mashtaka kwa watuhumiwa na kuwafikisha mahakama ya mwanzo, hivyo kushusha hasira ya wananchi hao.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Tunduma mheshimiwa Frank Mwakajoka Mwesa,ambaye alikuwa mmoja wa waalikwa kwenye mkutano huo amesema amesikitishwa na kitendo cha wananchi hao kushtakiwa mahakamani kwani hakuona kitendo chochote cha sambulio na kwamba hawezi kuingilia uhuru wa mahakama anaiachia itende haki.

Wakati kesi hiyo ikitajwa mahakamani hapo mlalamikaji  Bwana Cheyo,hakuwepo mahakamani na pia hakuwa tayari kuzungumzia lolote kuhusiana na kesi hiyo.

Kata hiyo imekuwa na migogoro ya mara kwa mara hivyo kufanya eneo hilo kuwa tete huku wanafunzi wakijazana katika vyumba vya madarasa na wengine wakisoma kwa kuchuchumaa madarasani.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger