Pages


Home » » WALEMAVU WANAPASWA KUTHAMINIWA NCHINI TANZANIA

WALEMAVU WANAPASWA KUTHAMINIWA NCHINI TANZANIA

Kamanga na Matukio | 05:23 | 0 comments

Tumefanikiwa kuangaza Vijijini na kutembelea katika Shule ya Walemavu ka Katumba 2 iliyopo Wilaya ya Rungwe, Mkoani Mbeya, jamani wanahitaji msaada ili naowajione wananafasi na mchango mkubwa wenye umuhimu katika jamii,
Sio kuwatenga, sio kuwaacha kwani sote ni sawa, kumbuka kuwa nao wanandoto kuwa kama huyu na yule.
Saidia kwa moyo wako kwa watoto hawa.
Sote yatupasa kuwa nao, tushirikiane kwa pamoja tuhakikishe nao pia wanapata elimu ya kutosha.(Picha na Kamanga na Matukio & Chimbuko Letu, Katumba - Mbeya)
******
Makala na Ester Macha, Mbeya.
Walemavu ni watu ambao wanatakiwa kuthaminiwa katika jamii kutokana na hali halisi ya maumbile yao waliyozaliwa nayo kuwa hivyo ,hakuna budi jamii hiyo ikapewa kipaumbele katika masuala muhimun hususani suala la elimu ambapo wengi wao wamekuwa nyuma kielimu.

Nadiriki kusema hivyo kwasababu mara nyingi jamii imekuwa ikiwasahau walemavu na kuatenga kutokana na jinsi walivyo na kusahau kuwa nao wana haki ya kuheshimiwa, kupendwa,kuthaminiwa kama watu wengine ambavyo wanajaliwa  na jamii.

Lakini cha kushangaza hali hiyo imekuwa tofauti kwa jamii hii ya walemavu ambapo baadhi ya kaya zimekuwa zikiwatenga watu hawa kwa kuwafungia ndani kwa kuona kuwa ni mkosi katika familia husika.

Vile vile hata wabunge na madiwani wamekuwa wakisahau  jukumu la kuwasaidia walemavu na kujikuta wakiendelea kusaidia wananchi wengine huku wakifahamu kuwa kuna kundi lingine la walemavu ambao wanahitaji msaada mkubwa hasa maeneo ya vijijini ambako wamekuwa na dhana ya kuona kuwa walemavu ni mkosi katika familia zao.

Nashauri viongozi waliopewa mamlaka ya kusaidia wananchi pia waone au kufika vijijini na kutambua kero mbali za walemavu na si kuwaangalia watu wanaojiweza pekee yao ambao ndio wameona ni msaada pekee kwao.

Huko vijijini kuna walemavu wapo ndani zaidi ya miaka 20 hawajawahi kutoka nje zaidi kukaa ndani tu,kama viongozi hawataweza kujua kero za wapiga wao kwa kuangalia pande zote mbili ambazo ni walemavu na wananchi wenye uwezo huku wakisahau kundi hili la walemavu ambao nao ni wapiga kura licha ya kuwa ni walemavu.

Nionanavyo kwa wabunge  na madiwani wajaribu pia kuwapa kipaumbile walemavu wa aina zote kuliko kuwasahau na kujikita zaidi na kundi moja tu ambalo ni wananchi ambao hawana tatizo lolote katika viungo vyao.

Katika pita pita yangu nimekuwa nikishuhudia mikutano au vikao vingi ambavyo vimekuwa vikifanywa na Wabunge na Madiwani  lakini kilichonisahangaza sijaona kati ya viongozi hawa aliyejaribu kukugusia kero za walemavu ambazo zinawakabili katika maeneo yao.

Jambo ambalo nimeliona na ambalo linatakiwa kuigwa na wabunge  na madiwani wengine ni hili la Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bw.Philipo Mulugo (Mb)kuweka kipaumbele kwa walemavu na wazee ambao hawajiwezi kimaisha kuwasaidia kila anapofika kufanya mikutano ya hadhara katika Jimbo hilo yote ni kuweza kujua kero za wananchi wote.

Nimemua kusema hivi si kwamba nimeamua kumpa sifa Mbunge huyu bali ni kutokana na utendaji wa kazi yake ya Ubunge ambao amekuwa akiufanya bila ubaguzi kwa kuona kuwa kuwa kundi maalumu la walemavu wote ambao wanastahili kupata huduma na kama watu wengine.
Kwa kutambua kundi hili mbalo mara nyingi limekuwa likitengwa na jamii  na hata wengine wameshindwa kutoka  ndani zaidi ya miaka 20 sasa Bw.Mulugo aliamua kutoa baiskeli 200  zenye thamani ya mil.50 kwa walemavu na wazee wote wa jimbo la Songwe .

Ninachokiona hapa ni kwamba  Mbunge huyu aliamua kufanya hivi baada ya kuona kuwa jimbo hilo la Songwe kuwa na idadi kubwa ya walemavu ambao hawakuw na msaada wowote na kuona umuhimu wa kuwasaidia wale walemavu ambao hawajaweza kutoka ndani kwa muda mrefu kutokana na hali halisi waliyonayo.

Si jimbo la songwe pekee lenye walemavu bali hata Jimbo la Mbeya lina walemavu wengi ambao wanahitaji vitendea kazi ili waweze kutembea na kufanya shughuli zao je nani wa kuwaona kama si viongozi wenyewe kuangalia makundi haya ambayo mara  kadhaa yamekuwa yakitengwa na jamii?

Nimekuwa nikishuhudia idadi kubwa ya walemavu wakiwa mitaani kuomba kuomba ili kuweza kujikimu kimaisha kutokana na hali duni waliyonayo ya kimaisha.

Ifike wakati viongozi wetu waliopewa mamlaka ya kusaidia wapiga kura waweke kipaumbele suala hili hata kwa kuwapatia mitaji ya biashara ili waweze kuendesha maisha yao kuliko kutegemea kupewa fedha kidogo ambazo haziwafikishi popote zaidi ya kuwaongezea ugumu wa maisha.

Sawa hata hili wazo la Mbunge wa Jimbo la Songwe la kuwasaidia baiskeli  si baya kwani kuna wengine ambao hawajiwezi kabisa kutembea kufika saehemu nyingine kujitafutia riziki hii nayo itakuwa msaada mkubwa kwao.

Nionavyo kwa upeo wangu msaada huu hautoshi pekee bali kinachotakiwa ni kupata nguvu nyingine ya kuwasaidia walemavu  ili nao waweze kujisaidia wenyewe kwa nguvu zao kwa kuwa wamepata vifaa mbavyo vitawawezesha kuweza kushiriki vema shughuli zote za kijamii.

Si kwamba napinga msaada wa Bw. Mulugo kwanza napongeza kw wazo zuri alilokaa na kufikiri kwamba kundi hili limekuwa likihitaji msaada mkubwa na pia ameona mbali kwa kuona kuwa walemavu mara nyingi ni watu ambao wanakuwa watengwa na jamii na hata viongozi waliowengi wamekuwa wakiwasahau kwa mchango wao.

Ushauri wangu kwa Bw.Mulugo ni kuongeza bidii zaidi kwa kutafuta mbinu mbali mbali za kuweza kuwsaidia walemavu wa jimbo lake ambao kwa sasa wamepata miguu ya kutembelea kikubwa kilichopo kwao ni Mbunge huyu  kuwatafutia mitaji ili wawez kufanya  shughuli zao wenyewe na si kukaa kutegemea kupata misaada.

Tatizo ni kwamba wabunge na madiwani walio waliowengi hawana tabia ya kuongelea masuala ya walemavu badala yake wamekuwa wakijikita zaidi kwa watu wa kundi moja tu na kusahau kuwa kundi la walemavu ni muhimu pia kulisaidia.

Wabunge wengine na madiwani igeni mfano wa Naibu Waziri wa Elimu ambaye kwa kiasi kikubwa ndiye amekuwa akijali zaidi kundi hili la walemavu kuliko wabunge wengine ambao wamekuwa  wakijali zaidi makundi mengine na kusahau kundi la walemavu.

Si kwamba wabunge hawa wengine wamekuwa hawaombi misaada kwa wahisani kusaidia wananchi wao lakini wanachokifanya wao misaada hiyo inaishia kwenye shughuli zao binafsi badala ya kukumbuka na wananchi waliomfanya akawa mbunge.

Na hata Bw. Mulugo pia amekuwa akikumbuka fadhila ambayo amefanyiwa na wananchi wake na kukumbuka kile anachopata kuwapatia wapiga kura wake hata kama kidogo.

Ni kwamba misaada pekee haitoshi bali kitu kingine cha muhimu kinahitajika ni kuisaidia jamii hii iweze kupata elimu kwani walemavu wengine wana uwezo mkubwa wa kielimu lakini tatizo ni jinsi ya kufikia  maeneo ya shule kutokana na  hali halisi ya maumbile waliyonayo.

Mbunge huyu mpango wake wa kusaidia walemavu ni mzuri lakini pia azidi kuboresha suala la elimu kwani kuna walemavu wengine bado wanahitaji zaidi kusoma misaada pekee haitoshi kwani watasaidiwa mpaka lini?

Lakini pia nimshukuru Bw.Mulugo kwa kufikiri mbali na kuona kuwa kuna haja ya kusaidia kundi hilo ambalo wabunge wengine hawajaweza kusaidia au hata kuuliza majimbo yao yana  walemavu wangapi,lakini Mbunge huyu awe mfano kwa kujali walemavu na wabunge wengine na madiwani waige mfano huu.

Kwa mpango huu utawafanya wabunge wote waonekane kujali makundi yote na si kubagua kama ilivyo kwa wabunge wengine kinachotakiwa kwa wao ni kuona umuhimu wa kusaidia makundi yote katika jamii na si kuangalia nafasi ya mtu katika jamii.

Sidhani kama  kuna wbunge wenye mawazo ya kusaidia  kundi hili wengi wa viongozi akifika kufanya mikutano yake hana haja ya kuuliza  kama kuna kundi la walemavu katika Jimbo lake hili linatakiwa kuanza kufanyika kwa kufuata mfano wa Mbunge wa Jimbo la Songwe ambaye ameanza kuonyesha njia kwa wabunge wenzake kuwa kunma umuhimu wa kusaidia kundi hilo.

Ninachotaka kushauri ni kuwa  wabunge na madiwani waweke kipaumbele makundi ya walemavu wa aina zote pale wanapotembelea majimbo yao na kufanya mikutano wawe na ajenda ya kuzungumzia masuala ya walemavu kwa kutambua kero mbali mbali ambazo zinawakabili katika maeneo yao kwani kuna wazazi wengine wamewaficha walemavu ndani kwa kuogopa aibu kwa jamii.

Ili hili lisiendelee kuna haja kwa viongozi kufanya haya ili walemavu waliofichwa majumbani waweze kutolewa nje na kusaidiwa  kwa kufanya hivyo kutafanya idadi ya walemavu wanaofichwa ndani kupungua na hata wale ambao walikuwa hawatembei wataanza kujishughulisha ili kujiongezea vipato na hatimaye kuacha kuwa tegemezi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger