Pages


Home » » KIWANDA CHA KUSINDIKA NYAMA KILICHOPO MKOANI MBEYA CHAPATA MATUMAINI YA KUFUFUKA.

KIWANDA CHA KUSINDIKA NYAMA KILICHOPO MKOANI MBEYA CHAPATA MATUMAINI YA KUFUFUKA.

Kamanga na Matukio | 02:41 | 0 comments
 Waziri Mkuu Mheshimiwa Pinda akiwa ameongozana na viongozi wa sekta mbalimbali wakiwemo wabonge, Mkuu wa mkoa na wengineo, katika Kiwanda cha kusindika nyama Jijini Mbeya.
******
Habari na Mwanishi wetu..
Kiwanda cha kusindika nyama kilichopo Mkoani Mbeya kilichotelekezwa na serikali kwa zaidi ya miaka 30 sasa kimepata matumaini ya kufufuka baada ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda kukitembelea na kutoa maagizo.

Katika maagizo yake Waziri mkuu Pinda amelitaka Shirika hodhi la Mashirika ya umma nchini (CHC) kuhakikisha viwanda viwili vya nyama vya Tanganyika Parkers vilivyopo katika mikoa ya Mbeya na Shinyanga vinapata wawekezaji kabla ya mwezi Desemba mwaka huu.

Aidha ametaka viwanda vinavyohusiana na usindikaji wa mazao ya wakulima ndivyo vipewe kipaumbele ili wananchi wa kawaida waweze kunufaika kutokana na vijana kupata ajira.

Awali, akisoma taarifa ya kiwanda hicho, Afisa wa Tanganika Parkers, Joseph Mapunda amesema kuwa ujenzi wa kiwanda hicho ulianza mwaka 1975 na ulipaswa kukamilika na kuanza kazi mwaka 1985.

Hata hivyo amesema kuwa ujenzi huo ulisimama mwaka 1978 kutokana na ukosefu wa fedha pamoja na taifa wakati huo kuingia vitani dhidi ya nduli Idd Amini wa Uganda.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger