Pages


Home » » MWALIMU MKUU SHULE YA MSINGI ATUHUMIWA KUUZA MBAO 241 ZA SHULE.

MWALIMU MKUU SHULE YA MSINGI ATUHUMIWA KUUZA MBAO 241 ZA SHULE.

Kamanga na Matukio | 05:22 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Mwalimu Lawrence Katindasa wa Shule ya Msingi Mtumbo - Ilembo, Kata ya Vwawa, Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya, ametuhumiwa kuuza mbao 241 mali ya shule hiyo.

Mwalimu mkuu huyo alipewa jukumu la kusimamia upasuaji wa mbao hizo na Kamati ya shule chini ya Mwenyekiti Tuya, na mara baada ya kukamilika kupasuliwa zitumike katika ukarabati wa shule hiyo, lakini mwalimu alikiuka na kuwauzia mafundi waliokuwa wakizipasua na pesa zote kuzitumia kwa maslahi yake.

Wapasuaji mbao hao walikamatwa na Mwenyekiti huyo wa kamati ya shule ambaye aliwapeleka kwa Afisa mtendaji wa mtaa Bwana Ally Nzowa, ambaye naye aliwapeleka Kituo cha Polisi.

Aidha, Mwalimu Katindasa alipoitwa alikiri kuwauzia wapasua mbao hao mbao 241 na baadae Polisi hao waliamuru suala hilo likamalizwe shuleni kwa kuwa mwalimu amekiri kosa na walipewa mbao hizo walidai kuwa ni malipo kutokana na kazi waliyokuwa wanaifanya shuleni hapo.

Baada ya kutoka polisi mafundi hao waligoma kuzirejesha mbao hizo shuleni kwa madai wamepewa na mwalimu mkuu huyo, lakini Mwalimu huyo alikiri atazirejesha baada ya wiki moja toka alipotakiwa kufanya hivyo Novemba 2011, lakini baada ya muda huo kufikana yeye kusindwa kuwasilisha mbao hizo aliomba aongezewe muda yaani mwishoni mwa mwezi Novemba.

Lakini hata hivyo alishindwa kufanya hivyo licha ya kuombwa mara kwa mara na kamati ya shule.

Baadhi ya wajumbe walipomtaka Mwalimu Mkuu Katindasa kuahidi ni lini atalipa walisema kuwa mwalimu huyo ni mhehe hivyo ana hasira anaweza kujinyonga  na kwa upande wake kudai kuwa anaomba asifuatiliwe mara kwa mara na mpaka sasa anaumwa.

Suala hilo lilifuatiliwa na Afisa mtendaji Bwana Nzowa ambaye amesema atalifikisha polisiili wale wote waliohusika na ufujaji wa mbao hizo wachukuliwe hatua za kisheria.

Hata hivyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika Mei 7 mwaka huu, mtaani hapo wananchi walikasirishwa na kitendo cha mwalimu huyo kutokana na hujuma huku alifahamu dhahiri kufanya hivyo ni kosa kutokana na kuaminiwa.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger