Pages


Home » » WAUMINI WA EAGT KANDETE WAMTUHUMU MCHUNGAJI KWA USHIRIKINA.

WAUMINI WA EAGT KANDETE WAMTUHUMU MCHUNGAJI KWA USHIRIKINA.

Kamanga na Matukio | 05:34 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
 Waumini 45 wa kanisa la EAGT(Evangelical Asemblies of God), Kandete Mwakaleli, Wilaya ya Rungwe,Mkoani Mbeya wameamua kujitenga na kanisa hilo lililopo chini ya Mchungaji Jaremia Mwamwaja wa kanisa hilo kwa tuhuma za ushirikina.

Sakata hilo limetokea Mei 27 mwaka huu katika ibada ambapo mtoto wa Mchungaji huyo aitwaye Lydia Mwamwaja kupanda madhabauni na kushuhudia kuwa yeye anajihusisha na ushirikina ndipo waumini haowalipotaharuki na kumwamuru mchungaji huyo aondoke kanisani hapo na familia yake lakini mchungaji alikataa.

Alipopekuliwa mtoto huyo wa mchungaji alikutwa na hirizi mkono wa kushoto, ambapo alikiri kuwa yeye anajihusisha na masuala ya kushirikiana.

Tukio hili ni lapili kutokea kanisani hapo baada ya lile la kwanza la mwaka 2008,ambapo familia hiyo ya mchungaji ilihusishwa na imani za kishirikina.

Kwa upande wake Mchungaji Mwamwaja, amesema kuwa yeye na familia yake hupendelea kuangalia ni mikanda ya Nijeria, ambapo hujifunza mambo hayo ya ushirikina.

Hata hivyo waumini wawili wa kanisa hilo waliamua kuondoka hivyo kusababisha kanisa kubaki na waumini wachache wengi wao wakiwa ndugu wa familia ya mchungaji huyo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger