Pages


Home » » WANAFUNZI WAJISAIDIA HAJA KUBWA NA NDOGO PORINI BAADA YA VYOO VYA SHULE KUJAA

WANAFUNZI WAJISAIDIA HAJA KUBWA NA NDOGO PORINI BAADA YA VYOO VYA SHULE KUJAA

Kamanga na Matukio | 05:15 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Wanafunzi wa Shule mbili za msingi Ilembo na Mtumbo, Kata ya Vwawa, wilaya ya Mbozi, mkoani Mbeya wamelazimika kujisaidia haza ndogo na kubwa porini na mashambani kutokana na vyoo vya shule hizo kujaa kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Hayo yamebainika baada ya kutembelea shule hizo mbili na kukuta maandamano makubwa kwa majirani waliopo mita chache kutoka shuleni hizo, huku baadhi ya wanafunzi wakipokea matusi na wengine kufukuzwa na majirani hao.

Wingi wa wanafunzi wanaosoma katika shule hizo wamekuwa wakipata usumbufu mkubwa huku wazazi wa vitongoji sita vinavyozunguka shule hizo, wamekuwa katika marumbano kwa takribani mwaka mmoja kutokana na baadhi kuchangia mchango wa shilingi 2,000 kwa kipindi chote bila sababu ya msingi.

Afisa mtendaji wa mtaa wa Ilembo Bwana Ally Nzowa amesema kati ya wananchi 4,442 waliotakiwa kuchangia fesha hizo shilingi 8,884,000  ni watu 592 wamechangia shilingi 1,184,000 hivyo kukwamisha kabisa shughuli za ujenzi wa vyoo hivyo na kati ya pesa hizo shilingi 43,500 zimetumika na salio halisi ni shilingi 1,140,500.

Hata hivyo Mtendaji huyo amebainisha kuwa wazazi wa mitaa ipatayo saba wamekosa moyo wa uzalendo kwa kuchangia pesa ambayo ni mitaa ya Kitovuni A, Kitovuni B, Matengu A, Matengu B, Majengo, Nsenya na Namleya.

Mkuutano huyo uliofanyika katika mtaani hapo na kusimamiwa na Mwenyekiti wa mtaa wa Ilembo B, Bwana Henry Singogo amewataka wazazi kulipa michango hiyo ifikapo mwishoni mwa mwezi Mei ili kukamilisha ujenzi wa vyoo hivyo.

Hata hivyo waliazimia yeyote atakayekaidi kuchangia pesa hizo achukuliwa hatua kali za kisheria ikiwa ni pamoja na kumfikisha mahakamani kwa kukwamisha maendeleo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger