Pages


Home » » RC MBEYA AWAPONGEZA WAANDISHI WA HABARI

RC MBEYA AWAPONGEZA WAANDISHI WA HABARI

Kamanga na Matukio | 05:00 | 0 comments
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bwana Abbas Kandoro akipokea tunzo yake kutoka kwa Mwenyekiti wa Mbeya Press Club Bwana Christopher Nyenyembe kutokana na ushirikiano anaoutoa kwa waandishi wa habari mkoani hapa katika Ukumbi wa Itemba Village wakati wa Kongamano la Uhuru wa Vyombo vya habari duniani ambalo hufanyika kila mwaka Mei 3.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bwana Abbas Kandoro akimkabidhi tunzo yake, Mwandishi wa Gazeti la Raia mwema Bwana Felix Mwakyembe iliyotolewa na Chama wa waandishi wa habari Mbeya Press Club, baada ya kushinda tunzo za Taifa zinazotolewa na Baraza la Habari Tanzania (MCT).
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bwana Abbas Kandoro akimkabidhi tunzo yake, Mwandishi wa Gazeti la Tanzania daima na mmiliki wa Blogu ya Kalulunga Bwana Gordon Kalulunga, iliyotolewa na Chama wa waandishi wa habari Mbeya Press Club, baada ya kushinda tunzo za Taifa zinazotolewa na Baraza la Habari Tanzania (MCT).
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bwana Abbas Kandoro akimkabidhi tunzo yake, Mwandishi wa Gazeti la Majira Bi Esther Macha iliyotolewa na Chama wa waandishi wa habari Mbeya Press Club, baada ya kushinda tunzo za Taifa zinazotolewa na Baraza la Habari Tanzania (MCT).
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bwana Abbas Kandoro akimkabidhi tunzo yake, Mwandishi wa Bomba FM na mmiliki wa Blogu ya Kamanga na Matukio Bwana Ezekiel Kamanga iliyotolewa na Chama wa waandishi wa habari Mbeya Press Club, baada ya kushinda tunzo za Taifa zinazotolewa na Baraza la Habari Tanzania (MCT).
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bwana Abbas Kandoro akimkabidhi tunzo yake, Mwandishi wa Gazeti la Majira Bwana Rashid Mkwinda iliyotolewa na Chama wa waandishi wa habari Mbeya Press Club, baada ya kushinda tunzo za Taifa zinazotolewa na Baraza la Habari Tanzania (MCT).

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Abbas Kandoro katika picha ya pamoja na Waandishi wa habari mkoani Mbeya, nje ya Ukumbi wa Itemba Village mara baada ya kumalizika kwa Kongamano la Uhuru wa Vyombo vya habari.(Picha na Mbeya Yetu).
********
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya mheshimiwa Abbas Kandoro ameipongeza tasnia ya habari mkoani hapa kwa mchango mkubwa katika uhabarishaji na uelishaji jamii.

Ameyasema hayo katika Kongamano la siku ya Uhuru wa Vyombo vya habari duniani, ambapo kimkoa sherehe hizo zimefanyika katika Ukumbi wa Itemba Village uliopo mtaa wa Veta jijini Mbeya Mei 3 mwaka huu.

Kandoro amewaasa wamiliki wa vyombo vya habari kuwawezesha waandishi wa vyombo vyao ili wananchi waweze kupata habari sahihi na kwa wakati muafaka, lakini alitumia fursa hiyo kuwaonya waandhishi wa habari wasifanye kazi yao kwa vitisho ili kuleta usawa katika jamii, kutokana na baadhi yao wamekuwa wakiwatisha baadhi ya wananchi wanaodhani wanatuhuma.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa Mheshimiwa Kandoro, amesema waandishi wa habari wasiridhike hapo walipo bali wajiendeleze kielimu ili kukuza fani hiyo.

Naye, Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa Christopher Nyenyembe, alimpongeza mkuu wa mkoa kwa ushirikiano anaoutoa kwa vyombo vya habari hali inayofanya kazi ya uandishi kuwa rahisi na wananchi kupata habari za uhakika.

Hata hivyo Bwana Nyenyembe alichukua fursa ya kumkabidhi Mkuu wa Mkoa cheti utumishi uliotukuka kutokana na mkuu huyo kuthamini mchango unaotolewa na vyombo vya habari mkoani hapa.

Katika kongamano hilo Nyenyembe alimuomba Mheshimiwa Kandoro kukabidhi vyeti kwa waandishi mahili wanane waliopata tunzo za uandishi bora nchini zilizotolewa na Baraza la habari Nchini (MCT).

Waandishi wa habari waliokabidhiwa vyeti na Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Kandoro ni pamoja na Esther Macha, Gordon Kalulunga, Keneth Mwazembe, Festo Sikagonamo, Ezekiel Kamanga, Felix Mwakyembe, Christopher Nyenyembe na Rashid Mkwinda.

Kwa kutumia mchango wa waandishi wa habari hao na kuleta heshima kubwa kwa mkoa mheshimiwa Kandoro, amesema atatoa shilingi laki moja kwa kila mwandishi ili iwe chachu kwa wengine ili kufanya kazi kwa weledi mkubwa na hivyo kuongeza juhudi katika tasnia nzima ya habari mkoani hapa.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger