Pages


Home » » VIONGOZI WAJIMILIKISHA ARDHI WILAYA YA MBARALI.

VIONGOZI WAJIMILIKISHA ARDHI WILAYA YA MBARALI.

Kamanga na Matukio | 03:31 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbarali.
Viongozi 7 wa Kijiji cha Itamba, Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya wanatuhumiwa kuuza ardhi ya kijiji hicho kwa wafanyabiashara na wao kujimilikisha sehemu kubwa ya ardhi hiyo kinyume na makubaliano.

Hayo yamebaika baada ya kutembelea Kijiji hicho na kukutana na wananchi zaidi ya 200, ambao wameulalamikia uongozi wa kijiji hicho.

Viongozi waliotajwa na Mwenyekiti wa Kijiji Bwana Venance Magiye ambaye anadaiwa kumiliki hekari 35, Afisa Mtendaji wa kijiji Bwana Damson Simasilya hekari 10, Mwenyekiti wa ulinzi Bwana Ally Mpwaga hekari 20, Mjumbe Bwana Aidan Sangula hekari 60.

Wengine ni Bwana Amir Mlamata hekari 20, Majulisho Mwandungu hekari 30 na Jackson Nyiboma hekari 15 ambao wote ni wajumbe.

Ili kuleta usawa katika makubaliano ya mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo miaka 3 iliyopita waliridhia kila mwananchi apate hekari 2 kwa gharama ya shilingi 2,000 kila hekari.

Aidha, mbali ya kujimilikisha hekari hizo zote viongozi hao wanadaiwa kuuza ardi ya kijiji kwa wananchi zaidi ya 11 wasio wakazi wa kijiji hicho cha Itamba.

Mtandao huu umebahatika kunasa wahusika na hekari walizonunua ambapo Bwana Maso ameuziwa hekari 100, Bwaba Samike hekari 20, Bwana Gorogobo hekari 10, Mwalimu Amani hekari 10, Bwana Mbule hekari 20, Bwana Mabeva hekari 18.

Wengine ni Bwana Kilembe hekari 10, Bwana Seti Mhemeji hekari 10 wote ni wakazi wa Kijiji cha Mabadaga, Bwana Majiva wa Kijiji cha Ukwavila ameuziwa hekari 20 na Bwana Chaina wa Kijiji cha Itamba hekari 10.

Hata hivyo katika kuonesha kujichukulia madaraka mmoja kati ya viongozi Bwana Amir Mlamata aliuza shamba la Kijiji kwa gharama ya shilingi 1,300,000 kwa Bwana Kilangila Dotto (67) mkazi wa Itamba bila hata kutoa stakabadhi.

Kwa upande wake  Myenyekiti wa Kijiji hicho Bwana Magiye amesema kuwa yeye hajauza isipokuwa ardhi hiyo baadhi yao walishindwa kuiendeleza, hivyo walipewa watu wengine, lakini hakubainisha ni wakazi wa kijiji hicho au la na kwamba atatoa ufafanuzi katika mkutano utakaofuata.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger