Pages


Home » » MBUNGE WA VITI MAALUM WA MKOA WA MBEYA ASHIRIKI KONGAMANO LA MAOMBI DHIDI YA KUKOMESHA VITENDO VIOVU

MBUNGE WA VITI MAALUM WA MKOA WA MBEYA ASHIRIKI KONGAMANO LA MAOMBI DHIDI YA KUKOMESHA VITENDO VIOVU

Kamanga na Matukio | 03:34 | 0 comments

Mbunge wa Viti Maalum wa Mkoa wa Mbeya mheshimiwa Dakta Mary Mwanjelwa, akiongea na wananchi wa mwanjelwa  katika kiwanja cha sido, ambaye alikuwa Mgeni rasmi katika Kongamano la Maombi la kuuombea Mkoa dhidi ya Vitendo viovu.
*****
 Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Mbunge wa Viti Maalum wa Mkoa wa Mbeya kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dakta Mary Mwanjelwa, ameshiriki kongamano la maombi dhidi ya kukomesha vitendo viovu Mei 5 mwaka huu.

Kongamano hilo lililoandaliwa na Kipindi cha Faraja yako kinachurushwa alfajiri na usiku, kupitia Kituo cha redio cha Bomba FM kilichopo mkoani hapa na kufanyika katika Ukumbi wa St Mary uliopo Forest Mpya jijini Mbeya.

Kongamano hilo lilifunguliwa na Askofu wa Kanisa la P.A.G (Pentecost Assemblies of God) Damianus Kongolo Thomas, likiwa na nia ya kufanya maombi ya kukomesha vitendo viovu vinavyofanyika mkoani hapa ikiwa ni pamoja na Upigaji ndondo, ushirikina na ujambazi.

Askofu huyo alimpongeza Mbunge huyo Dakta Mwanjelwa, kwa kukubali wito licha ya kuwa na majukumu mazito ya kulitumikia taifa hivyo angeweza kutoa udhuru wowote, lakini pia alimheshimu Mungu kwa kujumuika na waumini wa madhehebu mbalimbali.

Aidha Mmoja wa watangazaji wa kipindi hicho Bi Martha Haule alisoma risala na kuelezea umuhimu wa kipindi hicho ambacho kinagusa jamii mkoani hapa kwa kutembelea wafungwa gerezani, wagonjwa hospitalini, vituo vya kulelea watoto yatima na waishio mazingira hatarishi na kutoa wito kwa mgeni rasmi na wananchi mbalimbali kuwatembelea wahitaji hao kwani ni upendo aliotuachia Bwana Yesu Kristu.

Akijibu risala hiyo Mgeni rasmi Dakta Mwanjelwa, amesema ameguswa na huduma nzito inayotolewa na kituo hicho cha redio kwani wanaigusa moja kwa moja jamii na kusema kuwa wanaisaidia Serikali na kiasi kikubwa na hii inaonesha jinsi gani watanzania walivyo na upendo ambapo kwa upande wake anaungana na kipindi hicho hivyo aorodheshewe vipindi vinavyohitaji msaada.

Hata hivyo Bomba FM redio hivi karibuni imefanya harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa kituo cha kulelea wazee ambapo jumla ya shilingi milioni 20 zilipatikana kwa njia ya kutoa papo hapo na nyingine kwa ahadi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger