Pages


Home » » ALIYEZIKWA AKIWA HAI HATIMAYE AZIKWA TENA.

ALIYEZIKWA AKIWA HAI HATIMAYE AZIKWA TENA.

Kamanga na Matukio | 04:12 | 0 comments
Kaburi la Nyerere Kombwee (52) (kulia) aliyezikwa akiwa hai, ambapo alifukuliwa na Polisi na baadae mwili wake kuzikwa upya siku ya Jumapili Aprili 29, mwaka huu na kaburi la Mpwa wake Regnand Kombwee ambao wote walizikwa siku hiyo.
*****
 Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Nyerere Kombwee (52) aliyezikwa hai siku ya Jumamosi Aprili 28 mwaka huu majira ya saa tatu asubuhi amezikwa tena siku ya Jumapili, siku mojaa baada ya mwili wake kufukuliwa na Jeshi la Polisi saa moja baada ya kifo chake.

Marehemu huyo alizikwa akiwa hai baada ya kutuhumiwa kumuua mjomba wake marehemu Regnand Kaombwee, kwa imani za kishirikina hali iliyowapa hasira nduguze na hivyo kuamua kuchimba kaburi ambalo ilitakiwa azikwe marehemu aliyefariki kwa ugonjwa lakini badala yake akazikwa marehemu Nyerere, licha ya kuwasihi wamwachie na angewapa kitita cha shilingi 200,000.

Hata hivyo nduguze walizikataa na kuendelea kumzika kikatili huku mara kadhaa marehemu akifanya jitihada za kutaka kujinasua katika kaburi hilo kabla hajakandamizwa na chepeo la mchanga ambapo alivuja damu, ambapo aliendelea kuzilama huku akinuia kwa yeyote aliyemtendea ukatilihuo pindi akipona basi atakiona kwa maana kwamba atakufa.

Baada ya kifo chake Nyerere Kombwee Polisi walifika kijijini hapo na kuwatawanya wanaukoo kwa kupiga risasi hewani na kuupeleka mwili huo katika Hospitali ya Rufaa iliyopo Jijini Mbeya.

Aidha mara baada ya uchunguzi kukamilika Polisi waliutoa mwili kwa ndugu zake na mazishi ya ndugu hao yalifanyika kwa pamoja siku ya Jumapili Aprili 29 mwaka huu, kaburi la Marehemu Regnand likiwa kushoto na kutenganisha ambapo Marehemu Nyerere likiwa na kusimika mti mrefu wa mita tatu kwenda juu na mita mbili kushuka chini huku mwili wake ukiwa umekandamizwa sikioni na mti huo aina ya mkaratusi.

Kitendo hicho cha mtu kuzikwa akiwa hai kimelaniwa vikali na Chifu Roketi Mwanshinga, ambaye amesema hali hiyo isipokemewa watu watajenga chuki, visasi na mauaji ambayo yanaweza kuepukika na ametoa wito wa kushirikishwa pindi wanapoona kuwa tetesi ya vitendo vya kishirikina.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger