Pages


Home » » WATU WAWILI WAMEFARIKI KATIKA MAZINGIRA MAWILI TOFAUTI.

WATU WAWILI WAMEFARIKI KATIKA MAZINGIRA MAWILI TOFAUTI.

Kamanga na Matukio | 05:19 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Watu wawili wamefariki Mkoani Mbeya katika matukio mawili tofauti, likiwemo la mtoto kufariki baada ya kutumbukia mtoni wakati akicheza na wenzake.

Tukio hilo la mtoto huyo aitwaye Alfa Sadiki(2),limetokea katika Kijiji cha Lukululu,Wilaya ya Mbozi Mei 26 mwaka huu majira ya saa sita mchana.

Baba mzazi wa mtoto huyo Bwana Sadick Eliakimu Swajiamesema wakati tukio yeye alikuwa amesafiri kuelekea Tunduma.

Tukio jingine limetokea Kijiji cha Mbuyuni,Kata ya Mbuyu,Wilaya ya Chunya Salome Herman(20) alifariki dunia baada ya kupigwa na jiwe,alipokuwa akipitia njiani Mei 26 mwaka huu majira ya saa tatu usiku.

Katika tukio hilo Bwana Joseph Mwandyehe alikuwa na ugomvi baina yake na wenzie watatu katika eneo la Kilabu cha Mbuyuni, ndipo alipokuwa amelewa alichukua jiwe kwa nia ya kuwapiga wagomvi wake alirusha jiwe na bahati mbaya lilipowakosa basi moja kwa moja na kumkuta marehemu ambayea alisababishiwa majeraha.

Baada ya kupingwa jiwe hilo marehemu alianguka na kukimbizwa katika Kituo cha Afya Mbuyuni na kufariki Mei 27 majira ya saa nne asubuhi.

Wakazi wa eneo hilo mara baada ya kupata taarifa za kufariki, wananchi walitaka wamuue lakini aliokolewa na Katibu tarafa Romward Mwashiuya, kwa kumficha kayika nyumba ya kulalia wageni  kumuepusha kipigo kutoka kwa wananchi wenye hasira kali.

Bwana Jose[h alipelekwa katika kituo cha Polisi cha Chunya  Mei 17 mwaka huu.

Hata hivyo Kamanda wa jeshi la polisi Advocate Nyombi amethibitisha kutokea kwa matukio yote na kwamba uchunguzi kuhusiana na matukio haya.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger