Pages


Home » » KAMANDA NYOMBI AFANYIWA SHEREHE YA KUAGWA NA MJATA NA APEWA UCHIFU.

KAMANDA NYOMBI AFANYIWA SHEREHE YA KUAGWA NA MJATA NA APEWA UCHIFU.

Kamanga na Matukio | 05:49 | 0 comments
Pichani aliyekuwa Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi(wa pili kulia), ambaye ametawazwa kuwa Chifu na kupewa jina la Chifu Mwalyembe, akishikana mkono na Chifu wa kabila la Wanyiha katika sherehe ya kumuaga zilizofanyika katika Uwanja wa monesho ya Nanenane maarufu kwa jina la Uwanja wa John B. Mwakangale jana. Kamanda Nyombi amehamishiwa makao makuu ya jeshi hilo Jijini Dar es salaam.
Kamanda Nyombi akiwa na baadhi ya machifu wa makabila ya Mkoa wa Mbeya, jana katika sherehe ya kuagwa kwake.
Kamanda Nyombi akisalimiana na mmoja wa wanachama wa Chama cha Muungano wa Jamii Tanzania(MJATA).
Chifu Merere wa kabila la wasangu.
Baadhi ya wanachama wa Chama cha Muungano wa Jamii Tanzania(MJATA), waliohudhuria sherehe za kumuaga aliyekuwa Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapa Nyombi.
Mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari mkoa wa Mbeya(Mbeya Press Club), Bwana Christopher Nyenyembe, akizungumza jambo katika sherehe za kuagwa kwa Kamanda Nyombi.
Kamanda Nyombi(Kulia) akiwa sambamba na Mwenyekiti wa MJATA Chifu Soja Masoko.
Mwenyekiti wa MJATA Chifu Soja Masoko, akizungumza katika sherehe za kuagwa kwa Kamanda Advocate Nyombi.
Burudani haikuwa nyuma, Wanachama wa MJATA akisherehekea kutawazwa kwa Kamanda Nyombi kuwa chifu, ambapo jina hivi sasa anaitwa Chifu Mwalyembe.(Picha na Ezekiel Kamanga na Ronard Bahame).
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger