Pages


Home » » MAKALA YA HARAKATI ZA KUPINGA VITENDO VIOVU NA VYA KIKATILI MKOANI MBEYA

MAKALA YA HARAKATI ZA KUPINGA VITENDO VIOVU NA VYA KIKATILI MKOANI MBEYA

Kamanga na Matukio | 04:50 | 0 comments

 Mmoja wa wananchi waliojeruhiwa kwa kipigo kufuatia mapigano yaliyozuka katika Kijiji cha Chilulumo Wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya Bwana Daudi Sikali.
Mabinti waliodhalirishwa kijinsia baada ya kubakwa na watu saba walionadaiwa kushinikizwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Chilulumo, Wilaya ya Mbozi, Mkoani Mbeya Bwana Bruno Chipungu, huku wakishikiwa mashoka kutenda ukatili huo wa ubakaji kwa mabinti. (Picha na Maktaba yetu)
*******
Makala na Ester Macha, Mbeya.
Pamoja na serikali na asasi zisizokuwa za kiserikali kuendelea kupinga vitendo vya kikatili kwa wanawake lakini hali hiyo imeendelea kufanyika katika jamii kwa wabinti kufanyiwa vitendo vya kikatili na kidhalilishaji pasipo kuogopa mkondo wa sheria.

Vitendo hivyo kwa siku za karibuni vilianza kupungua kutokana na serikali kuingilia kati na vyombo vya dola na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali lakini hali hiyo imeonekana kuanza kurudi kimnya kimnya tena cha kushangaza viongfozi wa serikali za vijiji ndo wamekuwa wakishiriki katika unyama huo.

Kutokana na hali hiyo hivi karibuni wasichana wawili wa familia moja wamefanyiwa ukatili wa kinyama baada ya kubakwa kwa zamu hadi kupoteza fahamu na kundi la vijana waliovamia nyumbani kwao.

Katika tukio hili la kusikitisha kwa wasichana hawa limeonekana kufanywa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Chilulumo kwa kutumia vijana sita  ambapo mwenyekiti huyo alikuwa akitoa amri kwa  vijana hao kufanya unyama huo tena kwa kujiamini .

Kinachoonekana kuuma kwa tukio hili la wasichana kwa jinsi kiongozi huyu alivyoweza kutumia madaraka yake kufanya ukatili huo huku akisahau madfaraka aliyopewa na  serikali.

Viongozi wa serikali kama hawa tunajua wao ndio wa kwanza kukemea matukio haya lakini cha ajabu kiongozi huyu amegeuka kuwa samba badala ya kukemea tabia ya ubakaji inayofanywa katika jamii.

Katika hali ya kawaida kiongozi huyu hakustahili kufanya kitendo hiki cha kinyama na kama alikuwa analipiza kisasi kwa wazazi wa watoto hao hakustahili kufanya hivyo kwani inaonyesha ni jinsi gani kiongozi huyu asivyofuata maadili ya kazi yake  na inaonekana kuwa amekuwa akifanya vitendo hivyo kwa kutumia cheo chake isipokuwa ilikuwa haijagundulika.

Tukio hili limeonekana kuvuta hisia za wakazi wa Mkoa Mbeya na Wilaya ya Mbozi kwa kumlalamikia mwenyekiti huyu wa kijiji kufanya ukatili huo wa ajabu kwa wasichana hao wadogo ambao ni taifa la kesho.

Ninachoamini hapo ni kwamba Mwenyekiti huyo wa kijiji inaonyesha kuwa alikuwa analipa kisasi ambacho anajua yeye kwani kwa hali ya kawaida kwa wabinti wadogo kama hawa sidhani kama kuna jambo kati  ya wasichana hawa na mwenyekiti huyu kwa upeo wangu  na akili yangu nafikiri kuwa ni kulipa visasi kutokana na mwenyekitri huyo kuwa na tofauti na wazazi wa wasicchana hao.

Bila aibu Mwenyekiti  huyu aliamurisha vijana hao kuvunja nyumba hiyo majira ya saa 3 usiku akiwa na vijana na kuumuru kuwafunga midomo wasichana hao kwa kutumia shuka ambazo walikuwa wamejifunika ili wasiweze kupiga kelele.

Ni kweli azima yao ilitimia huku Mwewnyekiti huyo wa Kijiji akiwa amesimama pembeni wakati vijana hao wakiendelea kuwabaka wasichana hao kwa zamu mpaka pale walipopoteza fahamu kutokana vijana hao kuwa wengi. 

 Ninachojiuliza ni kwamba mwenyekiti huyu alipata wapi ujasili huu wa kufanya  kitendo hicho cha kinyama  na kama alikuwa akosana na moja ya familia ya wazazi wa watoto hao kwanini amuue kulipiza kisasi kwa watoto hao?.

Wasichana hawa wa familia moja wamewfanyiwa unyama ambao hawawezi kusahau katika maisha yao kwani hilo ni kovu ambalo haliwezi kufutika maishani mwao kwanza ndani ya akili yao tayari wameharibika kisaklojia .

Kwa tukio hili ambalo wamefanyiwa wasichana hawa kuna hatari ya kuwa wameambukiz ugonjwa wa ukimwi  na magonjwa mengine ya ngono. Ni wajibu wa Hospitali ya Wilaya ya Vwawa kuhakikisha wasichana hawa wanachukuliwa vipimo vyote  ili kujua kama wameathirika au wazima .

Ninachoshauri ni kwamba vyombo vya dola vihakikishe Mwenyekiti huyu anachukuliwa hatua kali za kisheria kwa unyama huu aliofanya hasa ukizingatia kuwa yeye ni kiongozi wa serikali ambaye anatakiwa kuwa mfano  lakini bado aliamua kufanya kitendo hicho bila aibu.

Tukio hili limefanyika marchi 11 mwaka  huu majira ya saa 3 usiku wakati wasichana hao ndugu wakiwa wamela chumbani kwao  na kufanyiwa ukatili huu uliomshirikisha Mwenyekiti huyu wa Kijiji .

Nionavyo mimi mashirika ya kutetea haki za binadamu yaingilie kati suala hili mpaka kujua mwi

sho wake kwani natambua kuwa mwenyekiti huyu hajakamatwa kutokana na tamaa zilizojengeka kwenye vyombo vya dola bila ya kuwa na huruma na watu wanaofanyiwa unyama huu.

Kwa uzito wa tukio hili jeshi la polisi halina budu kuweka tamaa pembeni kwa kuhakikisha kuwa mwenyekiti huyu anachukuliwa hatua pamoja na vijana sita walioshiriki kufanya unyama huo.

Sawa Mwenyekiti huyu tayari yupo kwenye mikono ya sheria je lakini ninachokiona hapa ni ni kwamba wanasubiri waliopatwa na kitendo hicho wasahau kasha tukio hilo linaendelea kupigwa kalenda tu kuwa ushahidi bado.

Ushahidi upi ambao unatafutwa na jeshi la polisi  wakati walengwa hao walimwona mwenyekiti wa kijiji hicho baada ya kuvunjwa mlango wa chumbani akiwa na vijana sita sasa kipi kitakuwa kinakwamisha wakati suala hilo  linajieleza.

Hata hivyo wasichana hao wakieleza kwa uchungu wakiwa katika hospitali ya Vwawa walisema kuwa walipoingia ndani, walimwona mwenyekiti wa kijiji hicho, akiwaamuru vijana hao kuwafunga macho kwa kutumia shuka waliyokuwa wamejifunika na kisha wakaanza kubakwa kwa zamu.

Mmoja wa wasichana hao aliyebakwa alisema yeye alibakwa na watu wawili  na kupteza fahamu fahamu, baada ya hapo sikujua kilichoendelea mpaka nilipozinduka alfajiri nikajihisi nina maumivu makali sana nadhani waliendelea kunibaka hata nikiwa sina fahamu na nilipozinduka nikamwona mwenzangu akiwa na hali mbaya zaidi.

Msichana mwingine alisema kuwa alibakwa na vijana wengi ambao walikuwa wakiamrishwa na mwenyekiti wa kijiji, baada ya kuwafunga usoni kwa kutumia mashuka yao ambayo walikuwa wamejifunika huku  mwenyekiti huyo akiwakataza kupiga kelele kwa vitisho vya kuwaua.

Lakini cha kushangaza tena Ofisa Mtendaji wa kata ya Chilulumo alikataa kutoa barua kwa wasichana hao kwa madai muda wa kazi umeisha, hii inaonyesha ni jinsi gani  viongozi hao wasivyojali matatizo ya wananchi wao hata ile huruma ya kuwaona wasichanma hao wakilia kwa uchungu lakini bado mtendaji huyo aliendelea kufunga ofisi yake.

Hata baada ya kufika hospitali Wasichana hao hawakupata huduma yoyote zaidi ya kupewa vidonge vya homa na kutakiwa kurudi nyumbani, huku wakisikia maumivu makali sehemu zao za siri.

Walisema siku iliyofuata walifika askari polisi wakiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Gabriel Kimoro na kuwahoji lakini hawakumkamata mwenyekiti wa kijiji hicho, licha ya kuwahakikishia kuwa alishiriki katika uhalifu huo.

Wasichana hao walisema kuwa pamoja na viongozi hao kuwaona wakiwa katika hali mbaya hawakuwapatia msaada wowote wa kuwapeleka hospitali.

Lakini pia kinachoonekana kushangaza ni kwamba pamoja na Mwenyekiti wa kijiji hicho na Ofisa Mtendaji kuonekana kushiriki katika tukiuo hilo lakini bado hawakuweza kukamatwa na jeshi la polisi kwa madai hawafahamu kitu kama hicho na badala yake walikamatwa watu wengine tu wakati wahusika wakuu wapo.

Hili jeshi letu linawekwenda wapi ,wasichana hao wamesema ukweli kuwa walioshiriki katika tukio hilo ni mwenyekiti na Mtendaji iweje washindwe kukamatwa wakati ushahidi upo?.

Nakuomba Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya wachukulie hatua  mwenyekiti na Mtendaji kuwa na uchungu kama hao ni watoto  wako kwanini ushindwe kuamini maneno ya wasichana hao unatafuta ushahidi upi ?.

Lini jeshi la polisi litabaini kuwa walishiriki wakati walengwa  tayari wamesema hao ndo walioshiriki ukweli upi unatafutwa ili polisi waweze kuamini ?kwa kufanya hivyo unasababisha matukio hayo yazidi kuendelea katika kata hiyo, na hata kama siyo hapo inaweza kutokea sehemu nyingine tofauti na hapo ifike wakati jeshi la polisi lifanye kazi yake kwa uaminifu na si kuumiza wanannchi .
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger