Pages


Home » » ASKOFU ANILIKISA CHEYO AWATAKA WAKRISTO KUJIENDELEZA KIELIMU.

ASKOFU ANILIKISA CHEYO AWATAKA WAKRISTO KUJIENDELEZA KIELIMU.

Kamanga na Matukio | 02:05 | 0 comments
Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo hicho Bwana David Mwankina (kushoto), akifuatiwa na Askofu wa Kanisa la Moravian Tanzania Alinikisa Cheyo, Mgeni rasmi Dr Victoria Kanama na Mkuu wa Chuo hicho cha Ualimu Eliackim Mtawa.
*****
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Askofu kiongozi wa Kanisa la Moravian Tanzania Alinikisa Cheyo, amewataka waumini kuthamini elimu ili kuleta tija katika jamii.

Ameyasema hayo alipokuwa akifungua maombi kwenye Chuo cha Ualimu cha Kanisa la Moravian Mbeya katika mahafali ya pili ya chuo hicho Mei 3 mwaka huu jijini Mbeya.

Akinukuu baadhi ya vifungu katika biblia Askofu Cheyo amesema wazazi na walezi wanapaswa kuwajengea msingi wa elimu vijana kwani ndio urithi utakao wasaidia maishani mwao, badala ya mali kwani mali huisha au kupotea.

Kwa upande wake mgeni rasmi Dr Victoria Kanama, ambaye ni Mkurugenzi wa Hospitali ya K'S iliyopo jijini hapa na pia ni Mkuu wa Bodi ya Chuo Kikuu cha TEKU, amewataka wahitimu kufuata maadili mazuri ya ualimu na hivyo kuwa mabalozi wazuri wa chuo hicho, ambapo pia alikazia suala la kujiendeleza kielimu zaidi na kutobweteka.
 
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger