Pages


Home » » WATU WAWILI WAFARIKI KATIKA MATUKIO MAWILI YA AJALI MKOANI MBEYA.

WATU WAWILI WAFARIKI KATIKA MATUKIO MAWILI YA AJALI MKOANI MBEYA.

Kamanga na Matukio | 05:17 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Watu wawili wamefariki dunia, katika matukio mawili ya ajali ya barabarani wilayani Mbarali na Rungwe, Mkoani Mbeya.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapa Advocate Nyombi amesema ajali ya kwanza iliyotokea katika Wilaya ya Mbarali, mei 20 mwaka huu majira ya saa 10 jioni barabara ya Mbeya/Iringa gari nambari T 536 APU likiwa na tela lenye nambari T 330 APD aina ya Scania.

Gari hilo lilikuwa likitokea Jijini Dar es salaam kuelekea mkoani Mbeya likiendeshwa na dereva aitwaye Ismail Kiteve iliacha njia na kupinduka kisha kusababisha kifo chake.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya hiyo iliyopo Rujewa, na chanzo cha ajali hiyo kimetajwa kuwa ni mwendokasi na upelelezi wa tukio hili unaendelea.

Aidha, Kamanda Nyombi amesema ajali nyingine imetokea Wilaya ya Rungwe majira ya saa 7 mchana, eneo la Katela barabara ya Mbeya/Tukuyu wilayani humo ikihusisha gari aina ya Toyota Coaster lenye nambari T 672 AWK.

Gari hilo lilikuwa likiendeshwa na dereva aitwaye Steven Mwambola(40), mkazi wa Mtaa wa Bagamoyo Tukuyu ilimgonga mwendesha pikipiki nambari T 628 BUL aina ya T-Better aitwaye Salim Jimu(26), mkazi wa Ntokela na kusababisha kifo chake papo hapo na abiria wake Gody Julius(17) kujeruhiwa.

Hata hivyo majeruhi huyo amelazwa katika Hospitali ya Mission Igogwe na dereva wa gari amekamatwa na gari lipo kituo cha polisi, kutokana na  mwendokasi uliyopelekea ajali hiyo na upelelezi wa tukio hili unaendelea.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger