Pages


Home » » WATU 6 WA FAMILIA MOJA WANUSURIKA KIFO BAADA YA MOTO KUZUKA.

WATU 6 WA FAMILIA MOJA WANUSURIKA KIFO BAADA YA MOTO KUZUKA.

Kamanga na Matukio | 05:22 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Watu 6 wa familia moja wamenusurika kifo baada ya moto kuzuka katika mtaa wa Ilolo, Kata ya Ruanda, Jijini Mbeya, Mei 17 mwaka huu.

Tukio hilo limetokea baada ya familia hiyo ya Bwana Ezekiel Mwasandube na mkewe Bi Christina Kyamba kulala na moto huo kuanzia sebuleni, ambapo inadaiwa kuwa dirisha la nyumba yao lilivunjwa na mtu au watu wasiofahamika kisha kuwasha moto kwa kutumia ufagio wa kupigia deki(mopu) ulionyunyiziwa mafuta ya taa na baadae kutokomea kusikojulikana.

Wengine walionusurika ni pamoja na Eva Mwasandube ambaye mwanafunzi wa kidato cha nne Shule ya Sekondari Sinde na Tabea Mwasandube ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha sita katika shule ya Sekondari Meta na William Mwasandube.

Wazazi walisikia yowe kutoka kwa watoto wao Eva na Tadea na walipojaribu kutoka kujua kulikoni ndipo wazazi walikumbana na wingu nzito la moshi ndipo waliomba msaada kwa majirani ambao walifika na kuvunja mlango na madirisha yaliyokuwa na vizuizi (grill) na kuwaokoa wanafamilia hao.

Baada ya tikio hilo Bi Kyamba na wanawe Eva na Tadea walizirai na kukimbizwa katika Hospitali ya Rufaa iliyopo Jijini Mbeya na hali zao zinaendelea vema.

Naye, Balozi wa mtaa Bwana Joseph Mwambapa na Mwenyekiti wa mtaa Benson Mbwana walifika haraka na kuwaomba wakazi wa eneo hilokusaidia kuzima moto.

Hata hivyo Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapa Advocate Nyombi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba Jeshi lake wanafanya uchunguzi kuhusiana na tukio hili.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger