Pages


Home » » MWENYEKITI WA KITONGOJI AUZA HIFADHI YA MBUGA NA PESA AWEKA MFUKONI MWAKE.

MWENYEKITI WA KITONGOJI AUZA HIFADHI YA MBUGA NA PESA AWEKA MFUKONI MWAKE.

Kamanga na Matukio | 05:21 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ilembo "A", Kata ya Vwawa, Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya Bwana Raphael Kibona, anatuhumiwa kuuza mbuga inayomilikiwa na mtaa huo kwa watu binafsi zaidi ya 30 na kufanya makazi ya kuishi tofauti na makusudio ya Kijiji na Serikali kwa ujumla.

Hifadhi hiyo ambayo hutoa chemichemi ya maji kwa Mto Mkusi Nkana na Mto Momba ipo hatariki kukauka kutokana na Mwenyekiti huyo kuendelea kuuza viwanja hivyo vya mbuga na pesa zote kujimilikisha licha ya malalamiko ya wananchi wa mtaa huo kumtaka kuacha mara moja.

Katika mkutano uliofanyika Mei 7 mwaka huu kijijini hapo, Mzee wa Kimila Bwana Witson Mwampashi, aliangua kilio kutokana na Bwana Kibona kutowaheshimu viongozi wa kimila na wananchi wa mtaa huo kwani muda wote waliitunza hifadhi hiyo ili iwe manufaa kwa vizazi na vizazi.

Aidha alipotaka kujieleza katika mkutano huo ni kwanini ameuza maeneo hayo ya mbuga mwenyekiti huyo alijibu kwa kujiamini kuwa ameshtukizwa swali hilo hivyo hayupo tayari kujibu tuhuma hiyo hali iliyofanya wananchi kutaharuki kabla ya kutumika busara za Mwenyekiti wa mkutano huo Bwana Henry Singogo ambaye aliwataka wananchi kuwa watulivu  ili watoe maamuzi ambayo yatasaidia mtaa huo kuokoa hifadhi hiyo.

Mara Kadhaa mtuhumiwa huyo aliitwa kwenye vikao vya mtaa na mara mbili kukiri kufanya makosa ya kuuza viwanja hivyo na kujimilikisha pesa mwenyewe na kuomba asamehewe.

Mkutano huo ulichrfuriwa na kauli ya Katibu tarafa wa Vwawa Bi Kasunga alipotumwa na Mkuu wa wilaya ili kutatua mgogoro huo na kuwa kauli yake ya kuwataka wananchi wapige kura kwamba Bwana Kibona asamehewe au la na baadhi kudai asamehewe.

Kutokana na kauli hiyo ya Katibu tawala wananchi hao walisema kuwa tangu lini mwizi akapigiwa kura pindi anapokiri kuiba, hivyo wametaka mtuhumiwa huyo akamatwe kwa kujipatia fedha kinyume cha sheria na hivyo uhujumu wa kiuchumi.

Mtendaji wa Kitongoji hicho cha Ilembo ameuambia mkutano huo kwamba yeye anajitahidi kuzuia eneo hilo lisiendelee kuuzwa lakini amekuwa akizungukwa na mwenyekiti huyo hivyo kuleta kero.

Kwa uchungu wananchi hao wamemtaka Afisa mtendaji kuorodhesha wale wote waliouziwa viwanja na gharama zake walizotoa ili pesa hizo ziwakilishwe kwenye mtaa huo na zisaidie ujenzi wa shule kijijini hapo ambazo ni shule ya Ilembo na Mtumbo ambazo zinaraslimali lakini hazina maendeleo yoyote licha ya kuwepo mji, hali baadhi ya wachache kujinufaisha.

Mkutano huo ulifungwa bila kuwa na muafaka na Mwenyekiti kukimbilia Godown kwa hofu ya kipigo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger