Pages


Home » » WAKAZI WAILALAMIKIA SERIKALI KUTOKANA NA KUSHINDWA KUDHIBITI VITENDO VYA UPIGAJI NONDO MKOANI MBEYA.

WAKAZI WAILALAMIKIA SERIKALI KUTOKANA NA KUSHINDWA KUDHIBITI VITENDO VYA UPIGAJI NONDO MKOANI MBEYA.

Kamanga na Matukio | 02:53 | 0 comments

Bwana Oscar Mbalamwezi (47) mkazi wa mtaa wa Chemchemi Kata ya Igawilo jijini Mbeya aliyepigwa nondo majira ya saa saba usiku wakati akitoka kuangalia mpira jana, akiwa amelazwa katika Hospitali ya Rufaa iliyopo jijini hapa.(Picha na maktaba ya mtandao huu)
******
Habari na Yohana Katema, Mbeya.
Wakazi wa Kata ya Iyela Jijini Mbeya wameulalamikia uongozi wa Serikali ya mtaa, halmashauri na jeshi la polisi kushindwa kudhibiti vitendo vya upigaji nondo pamoja na kuboresha miundombinu ya elimu na barabara.

Baadhi ya wakazi wa kata hiyo Lusekelo Mwalukasa, Ipyana Malangalila na Yusuph Mwakafilwa wamesema mara kwa mara wamekuwa wakitoa malalamiko ya ujenzi wa barabara, vyumba vya madarasa vya shule ya sekondari ya kata pasipo mafanikio ya aina yoyote.

Aidha wamesema licha ya zaidi ya watu 6 kupingwa nondo katika kipindi kifupi hakuna jitihada zozote ambazo wameziona zikichukuliwa na uongozi wa kata katika kuwapata wahusika wa natukio hayo.

Kwa upande wake Afisa mtendaji wa Kata hiyo Ezekiel Kipako, amesema suala la uboreshaji wa barabara linaendelea, ambapo barabara yenye urefu wa kilometa moja na nusu itajengwa kwa kiwango cha lami na suala la upigaji nondo upelelezi unaendelea ili kuwabaini wahusika wa watukio hayo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger