Pages


Home » » VIONGOZI 6 WATUHUMIWA KUFUJA MALI YA KIJIJI CHA NSONYANGA, WILAYA YA MBARALI MKOANI MBEYA.

VIONGOZI 6 WATUHUMIWA KUFUJA MALI YA KIJIJI CHA NSONYANGA, WILAYA YA MBARALI MKOANI MBEYA.

Kamanga na Matukio | 03:31 | 0 comments
*Watafuna maelfu ya pesa za kijiji,
*Ng'ombe aliyetolewa kama zawadi auzwa,
*Mabati ya msaada yachakachuliwa,
*Wakusanya pesa bila stakabadhi.
*******
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Nsonyanga, Wilaya Mbarali, Mkoani Mbeya Bwana Asumile Mtawa, anatuhumiwa kwa kufuja pesa za kijiji hicho kwa kushirikiana na wajumbe wa halmashauri ya kijiji na kushindwa kutoa taarifa za mapato na matumizi kwa zaidi ya miezi mitano.

Wengine wanaotuhumiwa katika sakata hilo ni Bwana Zacharia Mdolo(mtunza hazina), Kaisi Jonathan(M/kiti wa Kitongoji cha Nsonyanga), Anjela John(mjumbe), George Benard Mwambogo (M/kiti wa Kitongoji cha Mkoji), na Alimwene Saidi(mjumbe).

Lakini Asunile Mtawa na Kaisi Jonathan wanatuhumiwa kwa kuuza ng'ombe wa kijiji aliyetolewa na mwekezaji kijijini hapo Desemba 5, 2011 kwa ajili ya kufanya sherehe na lakini badala ya kufanya sherehe viongozi hao walimuuza na fedha hazikuwakilishwa katika mfuko wa kijiji.

Aidha Mtunza hazina wa kijiji hicho Bwana Mdolo, ambaye alipewa dhamana ya kutunza mabati 20, yaliyotolewa na mbunge mstaafu kwa ajili ya kujengea ofisi ya kijiji yeye kwa makusudi aliyatumia mabati 13 kwa matumizi binafsi na kubakia mabati 7.

Baada ya kubanwa na wananchi hao alifanikiwa kuyarejesha mabati 13 ya gauge 30, badala ya gauge 28 ya awali kinyume na ubora ambao umeidhinishwa na serikali kwani bati hizo zilinunuliwa mitaani na si katika bohari ya serikali.

Wakionesha kukasirishwa zaidi na ufujaji huo wa mali za kijiji wananchi hao, wamebaini kuwepo kwa uchakachuaji wa pesa za kijiji hicho mathalani kijiji kililipwa jumla ya shilingi 1,500,000 na mwekezaji lakini waliwasilisha shilingi 1,450,000, shilingi 800,000 zilikuswa kwa ajili ya mradi wa maji na zilipotakiwa ziliwasilishwa shilingi 300,000.

Aidha mchango kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu zilikusanywa shilingi 1,697,500 lakini ziliwasilishwa shilingi 1,060,000 pia shilingi 320,000 zilikusanywa kwa ajili ya mtaa wa Mkoji hazikuoneshwa kabisa.

Pia viongozi hao walikusanya shilingi 300,000 kwa ajili ya ukarabati wa Ofisi wa serikali ya kijiji lakini zilitumika shilingi 230,000.

Hawakuishia hapo viongozi hao walihujumu mbao zilizotolewa na mwekezaji kwa ajili ya ukarabati, na mbao 6 hazijulikani zilipo zenye thamani ya shilingi 36,000, mfuko wa saruji haifahamiki ulipo baada ya viongozi hao kupokea mifuko 10, wakahodhi lakini mifuko ilipodaiwa na wananchi ilikabidhiwa mifuko 9 tu ikidaiwa mfuko huo uliuzwa kwa ajili ya pesa za kumlipa fundi seremala.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mhongole Bwana Jandika Kisinza, amesema amesikitishwa sana na kitendo kilichofanywa na viongozi hao kwani wamekiuka kabisa maadili ya uongozi na kwamba ni kinyume kabisa cha sera za Chama Cha Mapinduzi, hivyo amewataka kurejesha mara moja mali hizo.

Mkutano huo ulisimamiwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Nsonyanga B, Bwana June Rasmus, Afisa Mtendaji wa Kijiji Medson Kilemile, Katibu mipango na fedha Mengo Rais, Erica Rams Mbogela, Daimon Njelwa, Juma Afrika Mwambopo(wote ni wajumbe) na Greyson Mololo, Anania Gervas, John Mwansaso, Ayoub Kabila na Martin Daud.

Mkutano huo ulianza kwa kupeleka muhtasari wa kikao kwa Mkurugenzi(w), Mbarali ili kupata muongozo wa hatua za kuchukua kwa viongozi waliohujumu Kijiji cha Nsonyanga.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger