Pages


Home » » MWENYEKITI WA KITONGOJI AIHAMA CCM NA KUELEKEA CHADEMA

MWENYEKITI WA KITONGOJI AIHAMA CCM NA KUELEKEA CHADEMA

Kamanga na Matukio | 04:59 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Mzimu wa viongozi wa Mitaa na Vijiji kukihama Chama cha Mapinduzi (CCM) na kuhamia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), umezidi kushika kasi baada ya viongozi wawili wa ngazi ya juu katika Kata ya Ilembo Wilaya ya Mbeya Vijijini, kukihama chama hicho tawala huku wakiongozana na wenzao sita Mei mosi mwaka huu.

Viongozi hao waliohama ni pamoja na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Moravian, Kijiji cha Shizuvi, Kata ya Ilembo Bwana Jongile Anosisye na Katibu wa CCM tawi la Shizuvi Bwana Yisambi Patikala, ambao wamesema wao kama viongozi wamechoshwa na kauli ya chama tawala ambazo hazitekelezwi.

Mathalani wameongeza kuwa waliahidiwa kupewa Kata kwa kipindi cha miezi sita tu, ukosefu wa barabara ya kutoka Ilembo hadi Shizuvi kwa muda mrefu.

Viongozi hao waliambatana na wanachama wengine 6 kuhamia CHADEMA ambapo ni pamoja na Bakulege Kwandende, George Tamali, Binoni Andambike, George Msabilwa, Mwakalebela Mwasenga na Raphael Mwasenga.

Aidha viongozi hao pamoja na wanachama walipokelewa na Katibu Kata wa chama hicho walichohamia Bwana Semi Mawingo na Katibu mwenezi Christopher Mwambamba na Mwenyekiti Bwana Daiman Mbeya.

Hata hivyo Katibu kata CHADEMA amesema hawajachelea kuhamia chama hicho kwani ndicho kitakacho wakomboa kifikra na mawazo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger