Pages


Home » » MIRADI 7 ILIYOGHARIMU MILIONI 407.3 YAFUNGULIWA WILAYANI MBARALI WAKATI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA.

MIRADI 7 ILIYOGHARIMU MILIONI 407.3 YAFUNGULIWA WILAYANI MBARALI WAKATI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA.

Kamanga na Matukio | 05:58 | 0 comments
  Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Peter Pinda akiwasha Mwenge wa Uhuru kitaifa jana katika Uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine ulipo jijini Mbeya. 
*********
Habari na Angelica Sullusi, Mbarali.
Jumla ya miradi saba inayogharimu kiasi cha shilingi milioni 407.3 imefunguliwa na Kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa Kapteni Honest Mwanosa, katika Wilaya ya Mbarali ambapo shilingi milioni 102.6 zimechangiwa na wananchi,milioni 39.2 fedha za halmashauri na milioni 265.4 zikitolewa na Serikali Kuu
 

Kapteni Mwanosa amefungua mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Kijiji cha Itipindi kata ya Mawindi kilichogharimu shilingi milioni 83.8 kilifunguliwa shilingi milioni 2.4 zikichangiwa na Halmashauri na Serikali Kuu ikichangia milioni 81.4. 
 
Banda la upimaji wa VVU kwa hiari katika kijiji cha Mkunywa lililogharimu shilingi milioni 2.5 fedha toka halashauri na nyumba ya mwalimu Kata ya Madibila iliyogharimu milioni15.5,milioni 14.5 nguvu za wananchi na milioni moja toka Serikali Kuu.
 
Pia ametembelea na kuweka jiwe la msingi katika miradi mingine ya maendeleo ya wananchi ambapo ujenzi wa vyumba vya madarasa sita katika shule ya sekondari Mshikamano Kata ya Igurusi vinavyogharimu shilingi milioni 44.2, shilingi milioni tisa imechangiwa na wananchi,milioni 32.4 kutoka halmashauri na milioni moja ikitoka Serikali kuu.

Miradi mingine ni ghala la kuhifadhia mazao katika kijiji cha Mbuyuni kata ya Mapogoro lililogharimu shilingi milioni 79.1 za wananchi, ufunguzi wa kituo cha raslimali kilimo katika kijiji cha Igomelo kilichogharimu shilingi milioni 150 fedha kutoka serikali kuu.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger