Pages


Home » » WAUGUZI WAINGIA MITINI BAADA YA MBIO ZA MWENGE - MBEYA

WAUGUZI WAINGIA MITINI BAADA YA MBIO ZA MWENGE - MBEYA

Kamanga na Matukio | 05:16 | 0 comments
 Zahanati ya Kijiji cha Mponwa,Kata ya Totowe,Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya iliyofunguliwa katika mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa,imetelekezwa baada ya Wauguzi wawili kuondoka siku nne baada ya kituo hicho kuzinduliwa Mei 12,Mwaka huu na Kiongozi wa mbio za Mwenge Keptani Honest Erenest Mwanossa.
Aidha,madawa mbalimbali ya afya za binadamu yamefungiwa ndani na funguo kukabidhiwa Afisa Mtendaji wa Kijiji na Mwenyekiti wake,ambapo dawa hizo zipo hatarini kuharibika baada ya popo na bundi kuvamia jengo hilo kwa ajili ya makazi.
Jiwe la msingi la ufunguzi wa Zahanati hiyo kama kinavyoonekana.
Baadhi ya dawa zilizotelekezwa na wauguzi baada ya kukiacha kituo cha kazi,siku nne baada ya mwenge wa uhuru kukizindua kituo hicho.
 Kwa habari zaidi endelea kufuatilia matandao huu(Picha na Ezekiel Kamanga)..
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger