Pages


Home » » AGOMA NDUGUYE KUZIKWA KATIKA JENEZA.

AGOMA NDUGUYE KUZIKWA KATIKA JENEZA.

Kamanga na Matukio | 05:19 | 0 comments

Habari na Ezekiel Kamanga,Mbeya.
Mkazi wa Kitongoji cha Mayewa,Kijiji cha Masanyila,Kata ya Igamba,Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya amegoma mwili wa nduguye  marehemu Onesha Nkota(Shilomanda) mwenye umri kati ya miaka 75 mpaka 80 kuzikwa katika jeneza.

Sakata hilo lililotokea Juni 27 mwaka huu majira ya saa nane mchana baada ya marehemu kufariki na Serikali ya kijiji chini ya Mwenyekiti  wake Bwana Nelson Mgode ulifanya jitihada za kuchonga jeneza lilogharimu shilingi 40,000 na kuliwasilisha nyumbani kwa marehemu kwa ajili ya maziko.

Lakini badala ya kushukuru kwa wanakijiji kwa msaada huo,ndugu huyo wa marehemu alilikataa akidai kuwa kutokana na umri mkubwa marehemu alikula madawa mengi,hivyo yataidhuru familia yake na kwamba juyo tayari nduguye kuzikwa kwa jeneza.

Aidha siku hiyo hiyo,baada ya familia kutafakarei kwa yote yaliyotokea waliamua kumuomba radhi mwennyekiti wa kijiji lakini alikataa,bali mwenyekiti alidai uitishwe mkutano wa hadhara aombwe mbele ya wananchi.

Kufutia hatua hiyo majira ya saa nane mchana mkutano uliitishwa na Bwana Mgode kuomba radhi na kutakiwa kulipa gharama zilizotumika kutengenezea jeneza na ng'ombe mmoka kama adhabu ya kuwadharau wanakijiji.

Hata hivyo Bwana Mgode alilipa gharama hizo na ng'ombe mmoja aliyechinjwa siku hiyo hiyo na jeneza kukabidhiwa katika uongozi wa machifu kwa ajili ya taratibu nyingine za kimila huku ndugu zake wakimlaumu kwa kuendekeza imani za kishirikina.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger