Pages


Home » » MTU MMOJA AKAMATWA AKIMILIKI SILAHA AINA YA GOBOLE KINYUME CHA SHERIA

MTU MMOJA AKAMATWA AKIMILIKI SILAHA AINA YA GOBOLE KINYUME CHA SHERIA

Kamanga na Matukio | 04:51 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga,Mbeya.
Wimbi la wananchi kujimilikisha silaha Wilaya ya Chunya,Mkoani Mbeya limeendelea tena baada ya mkazi mwingine wa wilaya hiyo kukamatwa akimiliki silaha kinyume cha sheria.

Bwana Felix Chombe(38) mkulima na mkazi wa Gua wilayani humo amekamatwa nyumbani kwake majira ya saa nne asubuhi Juni 14 mwaka huu,akiwa na silaha aina ya gobole.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa Diwani Athuman amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa anashikiliwa na jeshi lake pindi upelelezi ukikamilika atafikishwa mahakamani ili kujibu tuhuma zinazomkabili.

Hata hivyo ameongeza kuwa mtuhumiwa Bwana Shombe pia ni mwindaji haramu.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger