Pages


Home » » WAFUNGA OFISI YA MTAA BAADA YA MWENYEKITI KUKAIDI KUJIUZURU.

WAFUNGA OFISI YA MTAA BAADA YA MWENYEKITI KUKAIDI KUJIUZURU.

Kamanga na Matukio | 04:48 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga,Tunduma.
Wakazi wa mtaa wa Mwaka Kati,Kata ya Tunduma,Wilaya ya Momba,Mkoani Mbeya wameifunga Ofisi ya Mwenyekiti ya mtaa,kutonana na wananchi hao kuikataa taarifa ya mapato na matumizi.

Tukio hilo limetokea Juni 11 mwaka huu,majira ya saa tano asubuhi,wananchi hao waliamua kuweka kufuli jingine na kufanya ofisi hiyo kuwa na makufuli mawili,hali iliyopelekea mwenyekiti huyo kushindwa kuingia ofisini kwake.

Sakata hilo limekuja kufuatia mkutano wa hadhara uliofanyika mwishoni mwa mwezi Mei mwaka huu,uliokuwa na lengo la kusoma mapato na matumizi ya mataa kwa wananchi ambapo taarifa hiyo waliikataa iliyosomwa na Mwenyekiti wa mtaa huo Bwna Elias Cheyo na kumtaka ajiuzuru lakini alilikataa agizo hilo na kuondoka mkutanoni.

Kufuatia dhahama hiyo Mwenyekiti huyo aliamua kufungua mashtaka mahakamani na wananchi watatu wanashikiliwa kwa kosa la kutishia kuua kwa maneno,na kusomesha shtaka katika mahakama ya mwanzo Tunduma.

Aidha watu hao wamelikana kosa hilo hali ambayo ilipelekea kesi kuahirishwa mpaka Juni 11 mwaka ambapo mlalamikaji Bwana Cheyo,hakufika mahakamani hapo baada ya kutoa udhuru kwamba anaumwa.

Kesi hiyo imesogezwa mbele mpaka Julai 19 mwaka huu ndipo itakaposikilizwa tena katika mahakama hiyo.

Hata hivyo katika hali isiyokuwa ya kawaida wananchi kadhaa walionekana katika Mji huo wakiwa na mabango mbalimbali ya kulaani kitendo cha kutosomwa taarifa ya mapato na matumizi,hususani uvunjwaji wa kamati ya maendeleo ya ujenzi wa shule na ufujwaji wa pesa za makusanyo ya michango kutoka kwa wazazi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger