Pages


Home » » Wandishi tuliwatega wasanii kwa Sajuki, na sasa mwenzetu Athuman Khamis katutega………

Wandishi tuliwatega wasanii kwa Sajuki, na sasa mwenzetu Athuman Khamis katutega………

Kamanga na Matukio | 05:03 | 0 comments
Athuman Khamis, alipokuwa akirejea toka kwenye matibabu.

MHARIRI wa Picha wa Kampuni ya Tanzania Standard Newspaper Limited (TSN), Athumani Hamisi ameziomba kampuni, taasisi, wizara na watu binafsi kumsaidia ili aendeshe maisha yake.

Kwa takribani miaka minne, Athumani amekuwa akitibiwa baada ya mwili wake kupooza kutokana na ajali ya gari iliyoharibu uti wa mgongo aliyoipata Septemba 12, 2008 eneo la Kibiti, Pwani na kwenda kutibiwa kwa zaidi ya mwaka mmoja kwenye Hospitali ya MilPark ya Afrika Kusini.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Athumani alisema kwa sasa amekuwa anatumia kati ya Sh 750, 000 mpaka 900,000 kwa mwezi kwa ajili ya gharama za chakula, vifaa na gharama ndogondogo za wanafunzi.

Alisema kila mwezi anawalipa muuguzi na msaidizi wake Sh 370,000 na ada ya watoto watatu ambayo ni Sh milioni 2.4 ikiwa ni Sh 200,000 kwa muhula mmoja kwa mtoto mmoja.

“Maisha ya ulemavu ni ghali na sikutarajia hali hii. Nilikuwa nasaidia sana omba omba na yatima, lakini sasa nimekuwa ombaomba.

Ndugu wote wamenikimbia waliobaki ni marafiki wa kweli walioniingiza katika familia zao. Hali yangu ni mbaya sana kiuchumi,” alisema Athumani.

“Sina uwezo wa kulipa nyumba kwa gharama zozote zile, ninaomba Watanzania watakaoguswa wanisaidie nyumba na kwa ushauri wa daktari nimeshauriwa nisiishi mbali na mazingira ya hospitali,” alisema.

Msaada huo unaweza kupelekwa kwa akaunti namba za CRDB, 01J2027048800, Posta Benki namba 010-00090488 na kwa namba za mitandao ya simu za M-Pesa 0757825737, Tigo-Pesa 0655531188, Airtel Money 0784531188, M-pesa ya Chris Mahundi 0767298888 na Airtel Money ya Ephraim Mafuru namba 0686710977.

Aidha, Athumani alimshukuru Rais Jakaya Kikwete kwa kumtembelea katika Hospitali ya Muhimbili na kuagiza apelekwe nje kwa matibabu zaidi na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na pia kampuni anayoifanyia kazi ya TSN na waumini wa dini zote na marafiki zake waliohangaika.

“Ukweli ulio wazi, nashukuru kwa Mungu na kujivunia kuwa TSN.Nimelelewa na TSN kwa miaka sita sasa. Imenilea nikiwa mgonjwa kwa miaka minne, nikiwa bado niko ndani ya ajira jambo ambalo ni gumu sana sehemu nyingine,” alisema Athumani.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger