Pages


Home » » VIONGOZI WATAKIWA KUFANYA MAAMUZI SAHIHI KATIKA UTENDAJI WAO WA KAZI.

VIONGOZI WATAKIWA KUFANYA MAAMUZI SAHIHI KATIKA UTENDAJI WAO WA KAZI.

Kamanga na Matukio | 04:55 | 0 comments
Habari na Angelica Sullusi, Mbeya.
Imeelezwa kuwa maamuzi mengi yasiyo sahihi yanayofanywa  na baadhi ya viongozi hutokana na viongozi hao kukosa umakini na ubunifu katika kutoa maamuzi.

Akitoa mada ya Uongozi kwa wanasemina zaidi ya 30 kutoka katika Asasi isiyokuwa ya Kiserikali ya Taifa Kwanza Forum juzi katika ukumbi wa Bonanza uliopo eneo la Forest ya zamani Jijini Mbeya Dkt.Steven Mwakajumilo amesema kuwa wakati umefika kwa jamii kuelimishwa juu ya somo zima la uongozi.

Amesema kuwa changamoto kubwa waliyonayo viongozi wengi ni ya kutokubali kukosolewa na watu wa chini hata kama wamefanya makosa.

Aidha,Dkt.Mwakajumilo amesema kuwa viongozi wengi hupuuzia taarifa za tafiti mbalimbali ama kutofanya utafiti kabisa hivyo kuongoza kwa hisia zao binafsi badala ya tafiti  za kisayansi ili kusaidia kutatua changamoto mbalimbali za kijamii.

Pia ameongeza kuwa sababu nyingine ya kutopiga hatua za kimaendeleo husababishwa na viongozi wengi wenye dhamana kukumbatia vitendo vya rushwa na upendeleo pamoja na kujipatia utajiri wa kutisha kwa kujihusisha na mikakati hewa isiyo na tija kwa wananchi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger