Pages


Home » » WAKULIMA WA ZAO LA KAHAWA KUUZA ZAO HILO POPOTE.

WAKULIMA WA ZAO LA KAHAWA KUUZA ZAO HILO POPOTE.

Kamanga na Matukio | 03:57 | 0 comments
Mtafiti kutoka TACRI Bwana Dismas Pancras, akishika mche wa zao la Kahawa ulioathirika na ugonjwa unaoozesha mashina na mizizi unaitwa sterm and root rot unasababisha virusi vya vimelea vya Emilea melea vinavyoangamiza kabisa mimea ya kahawa na kuwa mikavu kabisa kama kuni.
*******
Habari na Mwandishi wetu.
Mgogoro kati ya kampuni ya Lima na vikundi vya wakulima wa kahawa kuhusu ununuzi wa zao hilo wilaya ya Mbeya vijijini umemalizika baada baraza la madiwani la halmashauri kuruhusu wakulima kuuza zao hilo sehemu yoyote wanayoitaka.

Akisoma taarifa ya utafiti iliyofanywa hivi karibuni wilayani humo mwenyejkiti wa kamati maalumu iliyoundwa kwa ajili ya kufuatilia mgogoro huo Msuba Luoakisyo amesema wakulima wamekuwa wakilalamikia kushuka kwa bei ya zao hilo, ununuzi holela pamoja na wizi wa kahawa zikiwa mashambani.

Katika kikao hicho cha dharula madiwani waliafikiana kutoa uhuru wa soko kwa wakulima kuuza kahawa, na kwamba msimamo wa bei ya zao hilo ibaki kuwa chini ya wakulima wenyewe.

Akihitimisha kikao hicho mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Mbeya na diwani wa kata ya Andason Kabenga ametoa pongezi kwa madiwani hao kufikia muafaka wa suala hilo ambalo limekuwa likisumbua kwa kipindi kirefu.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger