Pages


Home » » KIONGOZI WA SERIKALI ATUHUMIWA KWA KOSA LA KUFANYA UDANGANYIFU BENKI NA KUJICHUKULIA MAMILIONI YA PESA.

KIONGOZI WA SERIKALI ATUHUMIWA KWA KOSA LA KUFANYA UDANGANYIFU BENKI NA KUJICHUKULIA MAMILIONI YA PESA.

Kamanga na Matukio | 04:01 | 0 comments
Habari na Gabriel Mbwille,Mbeya.
Ofisa mtendaji wa Kata ya Nsalaga Bwana Cyprian Matola anatuhumiwa kuwadanganya watia saini benki na kuchukuwa shilingi milioni 2 na laki 8 za ujenzi wa sekondari ya kata kinyume cha taratibu.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti Kamati teule iliyoundwa kufuatilia ujenzi wa shule ya sekondari Uyole, Jelly Mwakipesile wakati akitoa taarifa ya kamati kwenye kikao cha Maendeleo cha kata hiyo.

Kamati hiyo iliundwa kutokana na kuwepo kwa taarifa, juu ya utaratibu mzima ambao haukuwa sahihi wa utoaji wa fedha benki na kupelekea kukwama kwa kazi hiyo ya ujenzi wa shule ya sekondari Uyole wakati fedha za ujenzi zilikuwa zimetolewa.

Aidha amesema fedha iliyokuwa ikichukuliwa benki na Ofisa Mtendaji Matola, ilikuwa inatunzwa UWAMU Saccos katika akaunti ya mtu binafsi hali iliyomfanya m,tendaji huyo awe anaizalisha fedha hiyo ya serikali kwa manufaa yake.

Nao wajumbe wa Kamati ya Maendeleo ya kata hiyo, walimtaka mtendaji Matola arudishe fedha hizo zilizotumika kinyume na taratibu na pia taarifa ifikishwe kwa Mkurugenzi wa jiji la Mbeya.

Jitihada za kumtafuta Mkurugenzi wa jiji, Juma Idd kuzungumzia suala hilo zimeshindikana kutokana na simu zake za kiganjani kutopatikana sanjari na kuwa nje ya ofisi kikazi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger