Pages


Home » » WANANCHI WAONYWA KUTOJICHUKULIA SHERIA MKONONI - MACHIFU MBEYA

WANANCHI WAONYWA KUTOJICHUKULIA SHERIA MKONONI - MACHIFU MBEYA

Kamanga na Matukio | 02:07 | 0 comments
 Mwenyekiti wa Muungano wa Jamii Tanzania(MJATA) Chifu Soja Masoko,akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Malamba,Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya,ambapo amewaonya kutojichukulia sheria mikononi dhidi ya watu wanaodhaniwa kuwa ni wahalifu au kwa mtu yeyote mhalifu.
 Wananchi wa Kijiji hicho.
 Bwana Simon Mbogo Mwatia ambaye ni mtoto wa marehemu aliyezikwa akiwa hai Rozina Mwadala(60),akiwa na Chifu Lyoto kijijini hapo.
Habari na Ezekiel Kamanga,Mbarali.
Mwenyekiti wa Muungano wa Jamii Tanzania(MJATA) Chifu Soja Masoko,amewaonya wananchi wa Kijiji cha Malamba,Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya kuaja mara moja tabia za wananchi kujichukulia sheria mikononi.

Ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji hicho Juni 15 mwaka huu,kufuatia kitendo cha wananchi wa kijiji hicho kumzika mkazi mmoja Rozina Mwadala(60) akiwa hai Juni 2 mwaka huu kwa kile kilichodaiwa kuwa alikuwa akijihusisha na imani za kishirikina.

Chifu Masoko amesema baada ya tukio hilo baadhi ya wananchi wamehama kijijini hapo kukwepa mkono wa sheria kuchukua mkondo wake,ambapo pia shughuli za kiuchumi zimezorota.

Aidha amewataka wananchi hao kurudi kwa hatua walizozichukua sio suluhu,hivyo warudi kijijini hapo na kukaa meza moja kujadiliana na sio kuamini baadhi ya waganga wa jadi wanaoendekeza vitendo vya upigaji ramli ambayo huchonganisha na kusababisha mauaji kwa wananchi wasiokuwa na hatia.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger