Pages


Home » » WATU WATATU WAFARIKI KWA AJALI ZA BARABARANI MKOANI MBEYA,MOJA WAKATI AKIJARIBU KURUKA.

WATU WATATU WAFARIKI KWA AJALI ZA BARABARANI MKOANI MBEYA,MOJA WAKATI AKIJARIBU KURUKA.

Kamanga na Matukio | 04:29 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga,Mbeya.
Watu watatu wamefariki katika ajali za barabara ni zilizotokea katika matukio mawili Wilaya ya Mbozi na Rungwe Mkoani Mbeya.

Ajali ya kwanza imetokea katika Kijiji cha Halungu,Wilaya ya Mbozi Juni 17 mwaka huu saa 1:45 asubuhi,ambapo lori lenye nambari T 801 BCJ aina ya Fuso mali ya Bwana Allan Mgula,mita chache baada ya kuvuka daraja la Halungu.

Dereva wa gari hilo Bwana Jestad Nyondo alipojaribu kumkwepa mpanda baiskeli iliparamia kifusi cha kokoto kilichoachwa barabrani kwa muda mrefu na mkandarasi wa barabara ya Mlowo.

Gari hilo lililokuwa na shehena ya mpunga na abiria 24 likitokea Kamsamba kuelekea Mlowo wilayani humo,limesababisha vifo vya watu wawili mwanaume na mwanamke ambapo majina yao hayajafahamika mara moja na majeruhi 20 kukimbizwa katika Hospitali ya Wilaya hiyo.

Miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali hiyo.

Ajali ya pili imetokea Kata ya Ikuti,Wilaya ya Rungwe Mkoani humo,ikihusisha gari nambari T 349 ABN aina ya Toyota Hilux Pick Up,baada ya kushindwa kupanda mlima wa Kinyika likiwa na abiria ambao idadi yake hakuweza kufahamika lilirudi nyuma ndipo baadhi ya abiria walianza kuruka kutoka katika gari hiyo.

Katika harakati hizo mmoja kati ya abiria hao ambaye ni mwanamke aliruka na kukanyangwa na gari kisha kupoteza maisha papo hapo na majeruhi mmoja ambaye ni mwanaume amelazwa katika Hospitali ya Makandana wilayani humo.

Hata hivyo Kamanda wa Polisi mkoani humo ACP Diwani Athuman amethibitisha kutokea kwa ajali hizo na kutoa wito kwa madereva kuwa makini wawapo barabarani na Jeshi hilo linajipanga kukabiliana na ajali za mara kwa mara.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger